Shule kongwe ya vipaji ya Kibaha sekondari yakabiliwa na uchakavu wa majiko ya gesi..wanafunzi wapo hatarini

 



SHULE kongwe ya vipaji maalumu ya wavulana Kibaha  Sekondari iliyopo Mkoa wa Pwani kwa Sasa  inakabiliwa na changamoto mbalimbali  ikiwemo  uchakavu mkubwa  wa majiko ya  gesi kuvuja hali inahatarisha usalama maisha  yawanafunzi pamoja na walimu kwani kunaweza kutokea  mlipuko na kupelekea majanga ya moto.




Changamoto hizo zimebanishwa na mmoja wanafunzi wakati akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake katika halfa ya mahafali ya kidato cha nne ambayo yamehudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na wadau katika sekta ya elimu.



Kwa upande wake Mkuu wa shule hiyo hakusita kuweka bayana madhara ambayo yanaweza kujitokeza kutokana na kuwepo kwa uchakavu huo na kuiomba serikali kuiangalia changamotoo hiyo kwa jicho la tatu.




Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo  ameahidi kushirikiana na serikali katika kuzitatua  baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo.




Naye  mkurugenzi wa Shirika la  Elimu Kibaha akawaasa wanafunzi hao kuhakikisha wanapenda na kuthamini masomo yao ili kutimiza ndoto zao katika suala la elimu.



Shule hiyo kongwe ya wavulana Kibaha sekondari ni yawanafunzi wenye vipaji maalumu ambapo viongozi mbali mbali wa ngazi za juu walishawahi kusomea hapo akiwemo Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikwete.



Post a Comment

0 Comments