MKANDARASI WA UJENZI WA BANDARI YA MBAMBA BAY AMETAKIWA KUMALIZA UJENZI KWA WAKATI



Na: Sheila Ahmadi


Naibu  Waziri wa Uchukuzi David kihenzile amemtaka   Mkandarasi   Xiamen Ongoing Construction Group Co.  Kutoka China anaejenga Bandari ya Mbamba bay  kumaliza ujenzi wa bandari hiyo kwa wakati kama inayoonyesha kwenye Mkataba.


Kihanzile ameyasema hayo  mara baada ya kutembelea eneo la Ujenzi wa Bandari ya Mbamba  bay  ambayo ujenzi wake unatarajiwa kukamilika Januari 2027 na kugharimu shilingi Bilioni 80.8.


"Nimeridhishwa na maandalizi ya Ujenzi wa Bandari hii hivyo  mnatakiwa kumaliza ujenzi wa bandari  kwa wakati kama inavoelekezwa kwenye Mkataba ili wananchi waweze kutumia bandari hii kibiashara na kunyanyua maendeleo ya Mbamba bay.’’ Alisema Kihenzile.


Aidha Kihenzile  amemtaka mkandarasi huyo   Xiamen Ongoing Construction Group Co. Ltd aweze   kuhakikisha anatoa ajira kwa vijana wa eneo hilo ili kuweza kupata ushirikiano mzuri katika utekelezaji wa Mradi huo .


Naye  Mbunge wa Nyasa Stella Manyanya ameishukuru serikali kwa Ujenzi wa Bandari hiyo  kwani utaweza kusaidia shughuli za kibiashara katika kukuza  ma eneo yaliyopo karibu ,pia ameomba kuboresha Miundombinu ya barabara katika eneo lote linalozunguka Bandari ya Mbamba bay.


Ametoa    taarifa  hiyo ya Mradi  Meneja wa Bandari ya Ziwa Nyasa Manga Gassaya amesema kuwa katika utekelezaji wa Mradi huo wametenga fedha  kiasi cha shilingi milioni miambili kwa ajili ya Ujenzi wa Shule ya Msingi karibu na  eneo la mradi  ambao  unatekelezwa


“Katika kushirikiana na jamii tumetenga shilingi milioni miambaili  kujenga shule iliyopo karibu Bandari  ili iendane na Ujenzi  wa bandari ya  inayojengwa Alisema Ngassaya.


Ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay ukimakilika inategemewa kuwa Kati ya Bandari kubwa katika ziwa Nyasa na kuwa makao makuu ya Bandari zote katika ziwa Nyasa  kwa Upande wa Tanzania.






Post a Comment

0 Comments