WAKALA WA MABASI YAENDAYO HARAKA (DART) WAMEHITIMISHA RASMI MAFUNZO YA TEKNOLOJIA YA TEHAMA KWA KUANZA KUTUMIA KADI JANJA.

 


Na Sheila  Ahmadi

Wakala  wa mabasi. Yaendayo haraka Dart wamehitimisha  Mafunzo rasmi  ya teknolojia ya Tehama.  kwa Waatalaamu na wengine.  wachache.  Lengo la mafunzo hayo ni kuweza  kujikita   kwenye.  kadi Janja Ambazo zinaenda kutumia kwa njia ya nauli kwa abiria ambao wanatumia mabasi hayo yaendayo haraka .


Hayo yamesemwa   Jijini  Dar es salaam   na Mtendaji  Mkuu wa wakala  wa mabasi yaendayo haraka Dart  Dkt Athumani   Kihamia alipozungumza na wana habari mara baada ya kufunga mafuzo hayo ambapo amesema  kuwa  kadi hizo za janja zitakuwa zinatumika kuingia  getini ili kuweza kulinda teknolojia ya  tehama  kwani   kuna baadhi ya watu wana tabia ya kudukua  kwenye  mifumo hiyo.


Dkt  Kihamia  amesema  kuwa lengo letu kwa sasa tunaimarisha  mifumo yetu ambayo  ilikuwepo huko nyuma  katika kuongeza  waatalamu wa teknolojia kwani watalaamu hao wamepata mafunzo. Mahiri  kutoka kwenye  kampuni ya Advanide  kutoka nchini  India ambao  wamekuja kutuwezesha  katika Mafunzo na kubadilishana  mawazo ya kitaaluma.


"Nichukue  Fursa hii  kuwaomba  Wantazania na wanadar Es salaam  waamini kuwa  siku chache zijazo baada ya Mwezi wa sita tunaenda   kuanza kutumia mageti yetu  kwani tumeleta  mageti   kutoka nje ya nchi yaitwayo  mageti janja zaidi ya 300. Ambapo mageti hayo yataenda  kutumika katika nauli ili kuweza kuepusha  kufuja kwa mapato na kuweza mazingira mazuri." Amesema Dkt Kihamia.


Nitoe  wito kwa Madereva boda boda  ambao wana tumia   barabara za mabasi yaendayo haraka   kuacha mara moja kwani  kipindi cha miezi ya nyuma kulikuwa na ajali nyingi   zinazosababishwa na madereva hao na wengineo wakiwemo katika kutumia barabara hizo Madereva daladala, wafanayakazi wa serikali hivyo acheni kutumia kipindi cha asubuhi na  jioni kwani mnasababisha ajali na foleni huku zikiwa na mabasi maalumu ya  kutumia njia hizo.


Naye  Mkurugenzi  wa Teknolojia, Habari. Na mawasialiano. kutoka Wakala wa  mabasi yaendayo haraka  Ng'wanashigi  Gagaga  ameongeza kuwa Mafunzo hayo yameweza kuchukua siku tano ikiwa na lengo ni kujenga uwezo Kupitia kwenye mfumo wa tehama ambao unatumia kadi janja  hivyo ni mwendelezo wa Mafunzo kwani huko nyuma tulishawahi kufanya Mafunzo haya kwa Mwaka 2020 kwa vijana 200  Huku  wengine wakifanya kazi Kwenye Taasisi mbalimbali.


Aidha ikumbukwe  kuwa Mifumo hii inayoenda kutumiwa na abiria limetengenezwa  na vijana ambao wameweza  kupata Mafunzo.hayo huku mageti hayo yanaenda   kusimikwa katika vituo kikiwemo kituo cha kimara korogwe kimesimikwa  mageti  kwa ajili  ya kufahamu   kuwa kadi ina fedha kiasi Fulani au hakuna kiwango cha pesa chochote kile " Amesema Mkurugenzi Gagaga


Kwa upande wake Mwezeshaji  wa Mafunzo kutoka  kwenye  Kampuni ya AdvanIde  Wa Kadi janja  Ducan    chege  amesema kuwa Huduma  hii ya kadi janja tunatoa sehemu mbalimbali.  duniani zikiwemo India,Tanzania  na nyinginezo  lakini kwa upande wa nchi ya TAnzania wamekuwa vinara katika  huduma hii ya kadi janja hivyo nawapongeza   kwa kuweza kutumia kadi janja kwa ajili ya Taasisi yao na abiria Kwa ujumla.


Kwa upande wake  Mhitimu wa Mafunzo hayo Jackson  Kazaura  amesema kuwa tumefanya Mafunzo haya ya kadi janja Ambayo yatasaidia  kwa upande wa wakala wa mabasi  hayo katika kuboresha huduma Za nauli na ulinzi katika vituo vya mabasi yaendayo haraka hivyo Mafunzo hayo yametujenga  kwa kiasi kikubwa

Post a Comment

0 Comments