Na Teophil Mbunda Dar es Salaam
Mwenyekiti wa chama cha ADC, Hamad Rashid Mohamed hii leo ametuma salamu za rambirambi kwa familia na chama cha TLP kufuatia kifo cha Mwanasiasa Mkongwe nchini, na Mwenyekiti wa Chama cha hicho
Ameyasema alipokuwa akizungumza ba waandishi wa habari kwenye Ofisi za chama hicho alipokuwa akifunguwa wiki ya kusherehekea miaka kumi toka kuanzishwa kwa chama cha ADC mwaka 2012
Augustino Lyatonga Mrema (77) ambae amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam.
Pole hiyo ameitoa leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa wiki ya miaka kumi ya chama hicho, ambapo amewataka watanzania kumuenzi Mheshimiwa
mrema kwani alikuwa na uwezo mkubwa katika masuala mbalimbali ya kisiasa
Msemaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Aminieli Eligaisha amesema, Mrema alilazwa hospitalini hapo kuanzia Agosti 16,2022 na kufikwa na mauti asubuhi ya leo Jumapili Agosti 21,2022 saa 12: 15.
"Alikuwa kiongozi ambaye ni nguli kwa siasa zetu za Tanzania, amepambana katika chaguzi mbalimbali na za vyama vingi vya siasa, Nitamkumbuka kwa mchango wake kwenye siasa za chama kimoja hadi vyama vingi. Pia
natoa Pole kwa familia na wana TLP. tuendelee kumuombea " Amesema Hamad Rashid Mohamed
Historia fupi ya nguli wa siasa nchini Hayati Mrema alizaliwa Desemba 31, 1944, Vunjo mkoani Kilimanjaro, amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, pia mgombea Urais kupitia NCCR-Mageuzi katika uchaguzi mkuu wa
mwaka 1995 ambao umekuwa ni uchaguzi wenye historia kubwa sana nchini kutokana na kuungwa mkono na Watanzania wengi na Baba wa Taifa Mwl. JK Nyerere, baada ya kujiunga na chama hicho akitokea Chama Cha
Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wakwanza wa vyama vingi.
Pia amewahi kuwa Mbunge wa Moshi Vijijini (CCM), Temeke (NCCR Mageuzi) na Vunjo kupitia TLP na hadi amefikwa na mauti alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole

0 Comments