Na. Sheila Ahmadi
Mamlaka ya mapato nchini Tanzania imeadhimisha siku ya Forodha duniani ikiwa na lengo la kuweza kuhamasisha. Ulipaji wa Jodi kutoka kwenye makampuni mablimbali na kuweza kulipa kodi kwa wakati kupitia biashara mbalimbali
Akizungumza na wanahabari Jijini Dar es Salaam Kaimu Kamishna wa Forodha, Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Hassan Juma amesema Maadhimisho hayo yameweza kufanyika Dar es Salaam kutokana na uwepo wa wadau wengi wa forodha na kuwatambua baadhi ya wadau ambao wanafanya kazi kwenye Taasisi mbalimbli za kiserikali na binafsi.
Kila. Inapofika. Januari 26 kila mwaka Idara ya forodha Tanzania inaadhimisha kwa mwanachama wote ambao wanafanya kazi kutoka kwenye Mamlaka hiyo ya Forodha Duniani hivyo kupitia TRA inaenda kuhamasisha ulipaji wa mapato nchini na kuendeleza uchumi wa nchi kutokana na kodi ambazo zinatolewa.
"lengo la maadhimisho hayo ni kwenda kutoa ujumbe kwa Umma juu ya shughuli. Ambazo zinazofanywa na Wadau wa Forodha nchini hivyo sisi Tunatambua umuhimu wa wadau hao ambao wameweza kushiriki katika kufanya shughuli hii ya forodha.
Aidha kamishina juma. Amesema kuwa mwaka huu Mamlaka ya Forodha Ulimwenguni (WCO), imetoa kauli mbiu ya Kutambua na Kuthamini juhudi na michango ya wadau mbalimbali katika kushirikiana na Wakala wa forodha nchini hivyo tumejipanga vyema katika kuhakikisha,na kutimiza majukumu ya kiforodha " Amesema.Kamishina Juma"
Hata hivyo amesema kuwa watawatambua wadau wa Forodha ambao wanafanyanao kazi ambao wanaweza kuwa Serikali, Makampuni binafsi, na Umma ambapo wataweka mazingira wezeshi ambayo yataenda kuwasaidia kutekeleza majukumu ya Kiforodha ambayo ni Kukusanya Mapato, Kusimamia mipaka na kuilinda jamii.
Vilevile utambuzi huo unatokana na majukumu ya kukagua bidhaa zinapoingia nchini ambazo haziruhusiwi lakini pia bidhaa zinazoingia nchini mpaka kupata vibali au ruhusa.
Forodha ina majukumu ya Mamlaka kubwa hapa nchini na ulimwenguni kote katika.kuweza kusimamia, kukusanya mapato ya Serikali na kulinda jamii ya watumiaji wa bidhaa mbalimbali.
Ukuaji wa Teknolojia nchini umeweza kusaidia mambo mengi yakiwemo ulinzi na usalama na sio kama zamani ilikuwa ni. kuwasilisha nyaraka kwa mkono kwa sasa hicho kitu ni historia hivyo zinaenda. Kutumwa kwa mtandao, ambapo unapata tathmini ya kila kitu pamoja na Kulipia.
Naye. Kamanda. Wa polisi kanda ya dar es salaam Jumanne. Murilo amesema ukaguzi wa Mizigo unatumia kifaa maalumu cha ukaguzi ambacho hufanya kazi kwa muda mfupi zaidi ambapo zamani ilichukua muda mwingi na rasilimali watu huku jeshi. La polisi likiwa na jukumu ya kulinda Amani ili kuzuia ubadhirifu wa Mali za watu.
Tunawakumbusha wananchi wafahamu thamani ya ulipaji wa kodi kwani nimekuwa nikifatilia kwa karibu mno wantazania wanapenda kutumia vitu vizuri ikiwemo huduma bora na vyenye thamani hivyo ulipaji wa kodi ni jukumu la kila Mwananchi kwaio wito wangu kwa wananchi ni kulipa kodi kwani tunaenda kujenga nchi .
Mchango wa jeshi la forodha katika maadhimisho hayo ni kuweza kuimarisha usalama wa nchi kwani tunataka wananchi wafanye vizuri biashara Zak na wawe katika mazingira wezeshi na pindi wapatapo faida waweze kulipa kodi. "Amesema. kamanda murilo
.jpg)
0 Comments