NAIBU WAZIRI WA UJENZI MHANDISI KASEKENYA AMETEMBELEA MADARAJA YALIYODHURIKA NA MVUA DAR ES ALAAM


Na  sheila  Ahmadi


Akizungumza  mara baada ya kutembelea daraja lililopo kunduchi  Mtongani    Naibu  Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya  amesema kuwa  madaraja ambayo   yamedhurika. na janga la mvua  serikali inaenda kuleta mawasikiano ya haraka kwa madaraja yote  ambayo yameharibika na kuwataka Wakala wa Barabara Nchini (TANROAD), kuhakikisha  kuwa wanakuja na mpango  madhubuti  wa muda mrefu wa kutengeneza njia sahihi ya maji.


Aidha  kasekenya  amewataka wahandisi mkoani humo  kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye kingo za madaraja hasa katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha nchini kwani mvua hizo zinaenda kupelekea changamoto kwa wakazi wa maeneo hayo.

Kutokana  na Mvua zinazoendelea kunyesha kwa sasa  wakala wa barabara  TANROADS  wanaendelea  kukagua miundombinu katika maeneo mbalimbali yaliyoathirika na mvua hizo ikiwamo Jangwani, daraja la Kunduchi na mengineyo 

"TANROAD   waanze  kufanya  ukaguzi  haraka iwezekanavyo ili waweze kuweka alama za tahadhari kwenye  barabara ili ziweze kwenda  kuwasaidia wananchi pindi athari zinapotokea.


Nyinyi TANROAD ndio wenye kujua changamoto na viashiria vya hatari, sasa ni vyema muwe mnafanya ukaguzi ili mtoe tahadhari ya haraka kwa wananchi  ili kwenda kuepuka madhara  mbalimbali yanayojitokeza kama haya ambayo yameweza  kujitokeza,” amesema Mhandisi Kasekenya.


Natoa  rai kwa wakazi  wa maeneo yote jijini dar  es saalam kuchukua tahadhari wanapopita katika maeneo ya madaraja, wakiona maji mengi na sehemu ya ardhi haionekani wasipite.


Niipongeze sana serikali ya awamu ya sita ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa maelekezo yake pindi Mamlaka ya Hali ya Hewa(TMA) ilipotangaza uwepo wa mvua hizi kubwa alitoa maelekezo kwa wizara zote kujiandaa na kukabiliana na changamoto zozote zitakazotokea ndio maana unaona changamoto hii ilipotokea wenzetu TANROAD makao makuu na mkoa wameshughulikia hizi changamoto kwa haraka,”amesema.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya wa Kinondoni, Saad  Mtambule ameipongeza TANROAD wa mkoa huo  na Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) kwa jitihada kubwa waliyoofanya za kurudisha huduma ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam.


Hata hivyo Mhandisi Suzana Lukasi amesema mvua imeharibu miundombinu ya madaraja na barabara lakini juhudi kubwa imefanyika ya kuhakikisha miundombinu hiyo inarejeshwa kwa wakati.


“Mvua hizi zilizonyesha zimesababisha uharibifu mkubwa lakini tumejitahidi kuhakikisha miundombinu hiyo tunairekebisha na sasa tumefungua njia zinapitika huku ukarabati mwingine.





Post a Comment

0 Comments