Na Sheila Ahmadi
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imeweka lengo la uhudumiaji wa makasha kwa asilimia 2.8 katika kipindi cha Julai hadi Desemba , 2023.
Akizungumza na Wanahabari na wahariri Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Plasduce Mbossa wakati akitoa ufafanuzi kuhusu utendaji na uendeshaji wa Bandari nchini kwa waandishi wa Habari.
Mkurugenzi mbosa amesema kiwango cha meli na shehena kwenye kipindi cha mwezi Julai hadi Di semba 2023 ni matokeo ya maboresho ya Bandari ambapo yaliweza kufanywa na Serikali ya awamu ya sita huku kupitia wizara ya mamlaka ya bandari TPA pamoja na kuimarika kwa Sera za uwekezaji nchini.
Kutokana na uboreshaji wa mazingira wezeshi kuwa kupitia Sera ya Diplomasia ya Uchumi inayotekelezwa na serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imeweza kuchangia ongezeko la Meli kupitia Bandari ya Dar es Salaam na kuendelea kuboreshwa kwa Bandari nyingine nchini na kuvutia wawekezaji katika kuendeleza uchumi.
Aidha amesema matokeo hayo ni jitihada ambazo zimefanywa na serikali katika kuimarisha uchumi wa nchi hivyo amepongeza kwa mikakati thabiti ya kukuza uchumi na Sera madhubuti za Uwekezaji nchini.
Vilevile amesema changamoto zilizopo katika mamlaka hiyo ya bandari ikiwemo muda wa upakuaji wa meli na udogo wa eneo hivyo kama wafanyakazi wameanza kuzifanyia kazi Kwa haraka ili kuongeza magati mengine 9 tisa
Suala la Bandari ya Bagamoyo amesema mradi huo unaendelea hivyo kwa sasa wanatangaza zabuni kwa mujibu wa sheria.
Naye mtendaji kutoka Bandari ya Dar es Salaam baada ya kuingia kwa Mwekezaji mpya mwaka huu kupitia kampuni ya DP-World wanaendelea na makabidhiano ya kisheria huku wafanyakazi wataamua kuendelea kufanya kazi TPA au kuhamia DP-World.



0 Comments