Na Sheila Ahmadi
Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki imefanya kongamano na wadau mbalimbali jijini dar es aalaam ili kuweza kupendekeza na kurekebisha sera mpya ya wizara hiyo katika kuweka maendeleo na vielelezo madhubuti hususani sera mpya katika wizara hiyo.
Hayo yamesemwa na Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa afrika mashariki Mh January makamba ambapo amesema kuwa katika kujenga sera mpya lazima tuwajibike katika lengo husika na kwenda kuleta Chachu kwa Maendeleo ya nchi.
Aidha Waziri makamba amesema kuwa katika kukusanya maoni hayo ya wadau ni kuhusisha marekebisho ya sera mpya kutoka kwenye wizara ya mambo ya ndani hivyo wadau ambao mmeshiriki kwenye kongamano hili ni vyema kwenda kuleta sera nzuri ambayo itakuwa inatumika kwa mambo mbalimbali.
"Amesema kama nchi inafanya mambo yaliyo sahihi lazima iweze kujikita katika ushawishi ikiwemo nchi ya Tanzania imejikita zaidi katika kufanya mambo ya ushawishi ambayo yataenda kulifanya nchi kuingia katika ubora wa hali ya juu "Amesema Waziri Mbarawa".
Waziri makamba amesema katika kufanyiwa marekebisho ya sera hiyo wizara hiyo imelazimika katika kufanya mabadiliko mbalimbali ambayo yametokea duniani kwa wakati huu hivyo imelazimu Nchi ya Tanzania katika kuendesha kwa mujibu wa mabadiliko hayo.
Katika hatua nyingine amesema katika mabadiliko hayo yakiwemo na tabia ya nchi kuibua Taasisi zenye nguvu na ushawishi wa uwezo wa kuweza kubadilisha vitu duniani hususani maendeleo ya teknolojia ya habari na mawasiliano na uwepo wa asilimia kubwa za wantazania waliozaliwa mwaka 2001 huku sera hiyo ikiwa imependekezwa.
Kutokana na hali hiyo wizara imeona vyema kufanya maboresho ya sera hiyo ili kuweza kutoa nafasi kwa wantazania wote na kutoa maoni yao juu ya sera hiyo na kuunda kesho yao ili kuendana na wakati wa sasa na wakati ujao.
Naye Naibu waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amesema msimamo wa Tanzania ni ule ule toka enzi za Hayati mwalimu Julius kambarage nyerere ni kushikamana na kuendeleza umoja katika kukuza sera nchini.
Kongamano hilo la kukusanya maoni ya wadau mablimbali ambao wamehudhuria litaenda kuleta chachu katika maendeleo ya nchi na kuibua viongozi Mahiri wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini wasomi na viongozi wa Dini kutoka mikoa Mbalimbali nchini.




0 Comments