WIZARA YA UJENZI YALETA MASTER PLAN KWENYE MIUNDOMBINU




Na  Sheila  Ahmadi


Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi imeaandaa Mpango Mkuu (Master Plan) wa Miundombinu ya nchi kulingana na mahitaji ya kiuchumi na kijamii itakayoweza  kurahisisha usafiri na usafrishaji wa bidhaa kutoka sehemu mbalimabli  kulingana na ongezeko la watu nchini.


Mpango huo unaenda kulenga  sababu mahususi kuhusu suala nzima la  barabara wa nchi nzima kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA).


 hayo  yamesemwa  na Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa, Jijini dar  es salaam wakati  alipokutana na Waziri wa Ardhi, Miundombinu, Usafiri na Utalii kutoka nchi ya Japan, Mhe. Konosuke Kokuba ambaye ameongozana na watalaamu mbalimbali wa Sekta ya Ujenzi nchini Japani.


“Miundombinu hiyo  ya barabara inaenda kuleta mafanikio  huku miundombinu mingine ikiendelea kufanya kazi kwa wananchi ikiwemo  reli, hivyo tunaenda  kushirikiana  kwenye   Wizara ya Uchukuzi ili kwenda  kuandaa master plan ya miundombinu katika  kuweza  kuhudumia watanzania”, amesema Waziri Bashungwa


Aidha  bashungwa ametoa  wito  kwa  TANROADS  katika  kuandaa majadiliano  muhimu  na Wakandarasi husika  kutoka Tanzania na nchi ya Japani ambapo watakuwa endelevu katika.kuendeleza  ushirikiano  wa  karibu katika Sekta hiyo.


Waziri Bashungwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa  maelekezo ya kuweka mazingira wezeshi kwa Wakandarasi Wazawa ambapo Wizara imeanza kupitia mpango wa manunuzi ambao  Mwanzo  ulikuwa unawakwamisha  wakandarasi hao.


Katika hatua nyingine  Waziri Bashungwa amepongeza Serikali ya Japani kwa  kwa kuonesha ushirikiano  Mahiri baina ya nchi hizo mbili  ambazo ni Tanzania na Japan hivyo    nchi ya Tanzania   itaendelea  kuzialika Sekta Binafsi kutoka nchi hiyo ili kuweza   kuendelea kufanya kazi na mkampuni ya Tanzania kwa karibu zaidi ili kubadilishana uzoefu  wa kazi




Bashungwa amesema Dhamira ya Waziri huyo ni kuja  kwa  muda sahihi kwani Serikali inaenda  kuboresha Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), kama mdau mkubwa wa matengenezo ya magari aina ya TOYOTA ambayo kwa asilimia kubwa yanatumika Serikalini na kuhitaji msaada wa kiufundi (Technical Assisatant).


Naye  , Waziri wa Ardhi, Miundombinu, Usafiri na Utalii kutoka Serikali ya Japan, Mhe. Konosuke Kokuba, amesema  Serikali hiyo itaendelea kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili  kwa kuendelea kujenga miundombinu yenye ubora katika miradi mbalimbali  inayoendelea na  ambayo inatarajiwa kutekelezwa  hivi  karibuni


Amesema  kutokana na  ongezeko la watu katika nchi zinazokuwa zinahitaji teknolojia za kisasa katika ujenzi wa miundombinu nchini ili ziweze kutosheleza kwa  mahitaji  muhimu kwa watumiaji


Sanjari na hayo Mkutano huo umeweza kukutanisha Taasisi za Wakala wa Barabara (TANROADS), Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), Wakala wa Majengo (TBA) na Jumuiya ya Maendeleo ya Miundombinu ya Japani - Afrika (JAIDA).

Post a Comment

0 Comments