NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI KIHENZILE- AITAKA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA (TAA) KUVUNJA MKATABA NA MKANDASI



Na  Mwandishi Wetu


Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile ameitaka mamlaka wa viwanja  vya ndege Tanzania (TAA) kuvunja mkataba na Mkandarasi anayejenga jengo la abiria la kiwanja cha ndege cha Ruvuma kutoka na Mkandarasi huyo kushindwa kukamilisha jengo hilo  kwa wakati.


Kihenzile ameyasema hayo Mara  baada ya kutembelea na kukagua maboresho makubwa ambayo  yameweza  kufanywa  kwenye  uwanja wa Ndege wa Songea mkoani ruvuma.


“Aidha Naibu waziri huyo  amesema kuwa Serikali imewekeza bilioni 37  katika  uwanja wa ndege  huu, hivyo ni muhimu jengo la abiria likamilike kwa haraka. Nauelekeza uongozi wa TAA kuvunja mkataba  na Mkandarasi anayejenga Jengo la Abiria kwani ameshindwa kukamilisha kwa wakati ,Alisema Kihenzile


Jengo hilo la abiria lilitakiwa kukamilika mwezi wa sita mwaka jana lakini mpaka sasa lipo asilimia 30 na Ujenzi wake unathamani ya shilingi milioni mianne ishirini na tatu (423) huku ujenzi  ukiwa  umesimama kutokana na  changamoto za mkandarasi huyo.



Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Songea  Kapenjama Ndile amesema kuwa uwanja wa Ndege wa Songea ni muhimu kwa  usafirishaji wa Mizigo na Abiria kutoka  nchi jirani kama vile Msumbiji na Malawi hivyo usafirishaji wa mazao ya Mboga mboga na matunda kama vile parachichi  hivyo wananchi wa Songea na Mikoa jirani ni Muhimu kutumia uwanja huu ,alisema  Ndile


 Awali  Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Songea   Mhandisi  Danstan Komba akisoma taarifa ya uwanja wa ndege huo amesema kuwa ujenzi wa Barabara ya ndege (Run way) umekamilika ,ujenzi wa barabara ya kiungio (Taxing Way) umekalika,Ujenzi wa kituo  cha nishati umeweza kukamilika  hivyo bado jengo la abiria .



Hata hivyo uwanja wa ndege wa Songea ni mojawapo ya viwanja vya ndege vilivyojengwa kuanzia mwaka 1974  kikiwa na barabara ya kutokana   na  kuruka ndege kwa kiwango cha changarawe, lakini sasa serikali umeboresha uwanja huo na kuwa uwanja wa kisasa.









Post a Comment

0 Comments