Na Mwandishi Wetu.
Mchambuzi wa maswala ya Siasa na uchumi Nchini, Bwana Kasim kibao Amesema kuwa mbunge wa kisesa Ndug luhaga mpina amefanya kitendo cha kupotosha umma juu ya tuhuma alizozitoa kwa Waziri Wa kilimo na chakula Mheshimiwa Hussein bashe ambapo amemtuhumu kwa kumuita fisadi kufuatia kutoa vibari vya uagizaji sukari kwa wafanyabiashara Biashara.
Hayo yamesemwa Jijini dar es salaam, na mchambuzi. Wa masuala ya kisiasa Kassim Kibao ambapo amesema kuwa kitendo alichofanya mh.mpina ni kukosa subra kwani alipaswa kufuata ushahuri wa Mheshimiwa spika bunge la jamhuri ya Muungano WA Tanzania Tulia Akson ambaye alimtaka kuleta ushahidi juu ya tuhuma hizo na nyingine mbalimbali.
Sanjari na hayo Kibao amesema kuwa kitendo kinachofanywa na mbunge huyo ni upotoshaji wa umma na kuleta taharuki kwa Wananchi jambo ambalo amesema ni kinyume na taratibu na Sheria za nchi.
Aidha. Kibao Amesema anachokifanya Mhe. mpina ni kutafuta huruma kwa Wananchi jambo ambalo sio nzuri kwani halina afya kwa Taifa letu la Tanzania.
Vilevile Kibao ameongeza kuwa kuhusu sakata Mheshimiwa Waziri wa kilimo mhe bashe ambaye aliagiza Wizara ya kilimo kutoa vibali kwa wafanyabiashara wa viwanda ili Kuokoa hali ya sukari Nchini katika kipindi cha mwezi mtukufu Wa Ramadhan na kwarezima.


0 Comments