VICTOR MASANGU,KIBAHA
Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe. Silvestry Koka katika kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta ya elimu ametumia fedha za mfuko wa Jimbo kiasi cha shilingi milioni tano katika mradi wa ujenzi wa shule ya msingi shikizi ya Saini ili kuondokana na changamoto ya wanafunzi wadogo kutembea umbari mrefu wa zaidi ya kilometa 12.
Hayo yamebainishwa na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Mathias Alexanda wakati akitoa taarifa kwenye ziara ya kikazi ya Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini ambaye alifika kwa ajili ya kuweza kutembelea miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu pamoja na miundombinu ya barabara.
Mkuu huyo amebainisha kwamba shule hiyo ambayo imeanzishwa mwaka huu imeweza kuwa ni kombozi mkubwa kwa watoto wadogo wenye umri wa kuanzia miaka mitano na kuendelea kutokana na hapo awali wanafunzi hao walikuwa na adha kubwa ya kutembea umbari mrefu kabla ya mradi huo wa shule kuanzishwa.
Mkuu huyo amempongeza kwa dhati Mbunge wa Jimbo hilo kwa kuweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni tano ambayo imeweza kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kuboresha miundombinu ya matundu ya vyoo pamoja na miundombinu mingine ya madarasa katika shule hiyo.
Kwa uapnde wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Silvestry Koka amebainisha kwamba lengo lake kubwa ni kuweka mikakati madhubuti ambayo itaweza kusaidia katika kuboresha sekta ya elimu hivyo ameamua kuchangia fedha hizo ili kuwaondolea wanafunzi hao kutembea umbari mrefu.
"Kikubwa nimefarijika kufanya ziaara ya kikazi katika kata ya Visiga na nimetembelea katika shule hii ya awali na darasa la kwanza na la pili la Saini na nimeweza kujionea mradi huu umeanza utekelezaji wake na ujenzi wa baahi ya madarasa na mm nimeweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni tano kwa ajili ya kuboresha sekta ya elimu ikiwemo madarasa pamojana matundu ya vyoo.
Aidha Mbunge Koka amebainisha kwamba kipaumbele chake kikubwa katika mfuko wa Jimbo ni kuhakikisha kwamba anaboresha zaidi shule ambazo zipo pembezoni ikiwemo kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya kuweza kuboresha zaidi miundombinu ya madarasa pamoja na maboma ambayo miundombinu yake imechaakaa.


0 Comments