SERIKALI YA TANZANIA IMEFANYA MAZUNGUMZO NA MAKAMU WA WAZIRI WA UCHUKUZI WA JAMHURI YA WATU WA CHINA.


Na  Mwandishi  wetu

 Waziri wa Uchukuzi Prof .makame Mbarawa  amefanya Mazungumzo   na Makamu wa waziri wa uchukuzi  Mheshimiwa Li Yang,  (Vice Minister, Ministry of Transport) kutoka  Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China. 


Prof  mbarawa amesema kuwa kutokana na masuala mengine,ya uzalishaji  tumejikita  zaidi  kwenye  majadiliano juu ya kuimarisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa njia ya Anga kupitia Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL). 


Aidha  kama  Tunavyofahamu  kuwa  ndege  ya Abiria ya Shirika la ATCL inafanya safari zake kwenda jijini Guangzhou, China mara tatu kwa wiki.  hivyo, kutokana na uhitaji  kuwa mkubwa, Tanzania imeiomba China kuongeza muda wa ndege hiyo  kuweza kuruka kwa siku zote za wiki ili kukidhi haja ya wasafiri wanaotaka kutumia ndege za Kampuni ya ATCL.


Vilevile  tumeweza  kuwasilisha ombi hilo, na  kuweka msisitizo zaidi kwa kuiomba Serikali ya Watu wa China kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya China (Civil Aviation Authority of China - CAAC) ili kwenda  kurahisisha mchakato wa kutolewa kibali kwa Serikali ya Tanzania cha kurusha ndege ya Mizigo aina ya Boeing 767-300 Freighter yenye uwezo wa kubeba tani 54 za mizigo kwenda Guangzhou angalau mara tatu kwa wiki. "Alisema Prof  Mbarawa"


"Kupitia mazungumzo hayo, Waziri Li Yang ameahidi kuharakishwa kwa mchakato wa upatikanaji wa ridhaa hiyo.


Katika   Hatua  nyingine  mbarawa  amesema kuwa  kwa Hatua ya upatikanaji wa kibali hicho itakapokamilika huku  zoezi la kupeleka ndege ya mizigo nchini China angalau mara tatu kwa wiki itapunguza changamoto  ya usafirishaji mizigo ambayo inawakabili Wafanyabiashara wa Kitanzania na kutoka nchi za jirani.


Pia  Kikao hicho  kimehudhuriwa na Mheshimiwa Khamis Mussa Omar, Balozi wa Tanzania nchini China, Mhandisi Ladislaus Matindi Mkurugenzi Mkuu wa ATCL na Viongozi wengine kutoka Wizara ya Uchukuzi na Taasisi za Wizara.

Post a Comment

0 Comments