Na Mwandishi wetu
Waziri wa Uchukuzi Prof Makame Mbarawa ameshiriki Kongamano la Kimataifa la Usafirishaji Endelevu (2024 Global Sustainable Transport Forum).ambapo Kongamano hilo limekutanisha Mawaziri na Wadau wa masuala usafiri kutoka Mataifa mbalimbali Duniani, huku likiratibiwa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kupitia Wizara ya Uchukuzi ya nchi hiyo.
Akizungumza Kwenye hadhara hiyo ya Mkutano Prof. Mbarawa ameeleza kuwa mafanikio na hatua mbalimbali ambayo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechukua katika sekta ya usafiri na usafirishaji ikiwemo utekelezaji wa miradi ya reli ya SGR, bandari ,na usafiri wa anga.
Aidha, Prof .Mbarawa, ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuonesha nia ya kuhusisha reli ya TAZARA ambapo makubaliano yake yalifikiwa tarehe 4 Septemba, Mwaka huu wakati wa Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali katika Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika- FOCAC. Ambapo Makubaliano hayo yalishuhudiwa na Marais wa Nchi za China, Zambia na Tanzania.
Katika Kongamano hilo Waziri Mbarawa amesema kuwa fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya uchukuzi zinazopatikana nchini inatumia jukwaa hilo kuwakaribisha wawekezaji wenye nia huku akiwahakikishia kuwa, Serikali ya Tanzania imeweka utaratibu mzuri wa kisera wa kushirikiana na Sekta binafsi katika kutekeleza baadhi ya miradi ikiwemo mradi Bandari na reli ya SGR ili kuwezesha kuifungua nchi zaidi kimaendeleo kupitia utaratibu wa Private Public Partnership (PPP).
Pia Hatua ambayo inaakisi mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Endelevu wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2030.
Sanjari na hayo Mbarawa ameongeza kuwa Kongamano hilo linalofanyika kwa siku mbili tarehe 25 na 26 Septemba, 2024 jijini Beijing, China, huku Waziri wa Uchukuzi akiwa ameambatana na Viongozi na Wataalam mbalimbali kutoka Wizarani na Taasisi za Sekta ya Uchukuzi.




0 Comments