RC CHALAMILA ATOA RAI KWA WANAOJIHUAISHA NA VIJIWE KWA MATUMIZI YA MADAWA YA KULEVYA

 

Na  Sheila  Ahmadi


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam  Albert  chalamila   ametembelea katika ofisi za mamlaka ya kudhibiti dawa za kulevya ambapo ametoa rai  kwa wamiliki wa  vijiwe hivyo ambapo  vinatumika kwa matumizi ya dawa hizo na kwenda kupelekea Athari mbalimbali kwa watumiaji .


Akizungumza na wanahabari  Jijini  Dar  es salam RC  Chalamila  alipotembelea kwenye ofisi hizo za udhibiti wa madawa ya  kulevya ( DCEA) amesema serikali itaendelea kushirikiana na mamlaka hiyo ili kwenda kutokomeza wahalifu ambao wanatumia madawa hayo kwani yanaenda kupelekea changamoto ya Afya na Akili  hususani mkoa wa Dar  es salam.


Amesema wahalifu  wengi  kutoka mkoani humo wanaweka makazi na vijiwe   kwenye maeneo ambayo ni hatarishi ikiwemo Eneo la Pemba mnazi kigamboni wahalifu hutumia eneo hilo kama kijiwe na kwa matumizi ya madawa.


Aidha  Chalamila amempongeza Kamishina jenerali

Kutoka  mamlaka ya udhibiti  wa madawa ya kulevya (DCEA )  Aretas  Lyimo kwa kufanya oparesheni  kubwa mkoani humo na kukamata madawa hayo ambayo yalikuwa yanaenda kutumika na wahalifu.


Naye  Kamishina Jenerali   Aretas  Lyimo  kutoka Mamlaka ya udhibiti wa dawa za kulevya amewataka viongozi wa dini nchini katika kuweza kushirikiana katika kutokomeza Janga hilo ambalo limekua  kero mkoani humo na matumizi holela kwa watumiaji wa madawa hayo.


"Ukamataji  mkubwa wa madawa hayo unaenda kupunguza matumizi ya dawa hizo katika kwenda kuondoa na kutokomeza kwa janga hilo nchini hususani mkoa wa Dar es salaam.  Amesema   Kamishina Jenerali  Lyimo.


Kwa upande wake Kamanda wa Polisi  kanda Maalumu ya Dar es saalam  Jumanne  Murilo  amesema mara kadhaaa katika kukamata wahalifu  hutokana na makosa ambayo hutokana na matumizi  ya dawa hizo za kulevya hivyo na kwenda kupelekea matukio mbalimbali yakiwemo Ubakaji, Wizi,   na Mauaji.


Kwa kushirikiana na Mamlaka hiyo Murilo amesema watahakikisha wanavunja vijiwe vyote maeneo mbalimbali ikiwemo maeneo ya ufukweni ambapo vinaenda kuleta Uhalifu nchini.


" sisi   kama  makamanda wa polisi kutoka  Dar  es salam Hatutokubali  Usaliti katika kupunguza suala hilo kwani yeyote ambaye atahusika katika uchochezi wa matumizi hayo ya dawa  haitomuacha salama sheria itachukuliwa na kufanyiwa kazi kwa wakati sahihi.





Post a Comment

0 Comments