SERIKALI IMEPOKEA VICHWA 3 VYA TRENI YA UMEME NA MABEHEWA 27 YA ABIRIA

 

Na:  Sheila  Ahmadi


Shirika la reli  Tanzania  TRC  limepokea vichwa vitatu vya Treni ya umeme  ambavyo vimeundwa na kampuni ya Hyundai Rotem na mabehewa mapya 27 ya kubeba abiria huku kampuni ya Sung shin Rolling stock Technology (SSRST) imeleta mabehewa hayo na vichwa vitatu kutoka nchini  Korea  Kusini huku serikali imefanya manunuzi ya vichwa vipya 17 na mabehewa mapya 59.


Hayo yamesemwa na  Kaimu mkurugenzi mkuu wa Shirika.la reli Tanzania (TRC) Mhandisi  Machibya masanja mara baada ya kupokelewa kwa  vichwa hivyo 3 na mabehewa 27  ya abiria  amesema mpaka sasa shirika limeweza kupokea vichwa vya treni ya umeme vinne  kati ya 17 kutoka kwenye kampuni ya Hyundai Rotem na mabehewa 56 kati ya 59 kutoka nchini korea kusini.


Mabehewa matatu  Ambayo yamesalia yanatarajiwa kuwasili nchini Mwezi Februari 2024 huku ikiwa vichwa 13 ambavyo vimebaki vinatarajiwa kuwasilli kwa awamu mbalimbali  vichwa sita vitawasili mwezi machi huku vichwa saba vitawasili Mwezi  April  2024.


Aidha  Mhandisi  masanja amesema vichwa ambavyo vimepokelewa kiutendaji vina uwezo wa Mwendokasi wa kilomita 160   kwa saa  huku mabehewa 27  yakiwemo  kwenye madaraja ya uchumi na Biashara daraja la biashara (Bussines class) ni mabehewa 13 ikiwa kila behewa lina uwezo wa kubeba abiria 45 na mabehewa ya daraja la uchumi (Economy class) ni 14 kila behewa lina uwezo wa kubeba abiria 78 kwa kuzingatia viwango vya kimataifa ili kuweza kumuwezesha abiria kusafiri kwa Amani na usalama."Amesema  Mhandisi  Masanja"


"Shirika hilo la reli Tanzania TRC  linaendelea kupokea kwa awamu vitendea kazi kea ajili ya uendeshaji  wa  reli  ya kiwango cha kimataifa (SGR)  na zoezi la majaribio  hayo ya vitendea kazi linaendelea  kwa mujibu wa Mkataba ili kuhakikisha vinaendana na mifumo ya miundombinu ambayo imejengwa nchini kabla ya kuanza uendeshaji wa kibiashara.


Kwa upande wake  Mkurugenzi  wa bandari ya Dar  es salaam  Mrisho  selemani amesema  kazi  ya kuhudumia bandari ni kazi yetu  hivyo suala la upokeaji wa vichwa na mabehewa hayo  limeenda kwa ufanisi  mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi  na kushirikiana na  shirika la reli Tanzania TRC  ili kuleta Huduma nzuri kwa wakati kwa abiria ambao wanatumia usafiri huo  wa Treni.








" Sisi   kama  watumishi wa bandari  tumeweza  kusimamia na kuhakikisha usalama wa vifaaa hivyo pasipo na kutokea  Ajali yeyote katika mapokezi ambayo yameanza kufanyika na hivi karibuni tunahitimisha zoezi hilo la mapokezi ya vifaa hivyo  huku serikali  ikiunga mkono kwenye suala hilo la kupokea mabehewa na vichwa  hivyo vya Treni.   "Amesema   mkurugenzi  Mrisho."

Post a Comment

0 Comments