VIFO VYA MAMA WAJAWAZITO VYAPUNGUA 85% MWAKA 2023 WAZIRI UMMY ATANGAZA

 

Na   Sheila  Ahmadi


Waziri  wa Afya  Ummy  Mwalimu  amesema vifo  vitokanavyo na mama  wajawazito  vimepungua kufikia hadi   %  85  kwa mwaka 2023 ambapo serikali imeweza  kutoa  huduma za afya huku maeneo 15  nchini  zikiwemo hosptali, Zahanati, na  Vituo vya Afya.


Akizungumza  Jijini  Dar  es salaam  waziri  wa afya Ummy  Mwalimu mara baada ya kutoa Taarifa  ya utoaji wa huduma za Afya  kwa 2023 ambapo wizara hiyo  imeweza  kutoa huduma nchini kote Mjini  na Vijijini  lakini huduma zitolewazo mjini ni tofauti na  kijijini  tunaamini  kuwa ongezeko la jitihada za watumishi zinaenda kuboreshwa mwaka huu.


Huduma za afya kwa mama na Mtoto  imeboeeshwa zaidi  katika mwaka uliopita ambapo wajawazito asilimia 97 wamehudhuria kiliniki katika kuweza kupata  huduma mara  nne katika kipindi cha ujauzito kwani ni muhimu kwa wajawazito katika kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.


"  Hatujafikia  malengo  madhubuti  kwani vifo vya akina mama wajawazito  vilikua 556 2023   kutoka elfu  11 kwa Mwaka na kuweza kuzuia  vifo hivyo na upasuaji wa dharura  wa kumtoa mtoto tumboni kwa  huku wanawake asilimia mbili wamejifungua   kwa njia ya upasuaji  "Amesema  UMmy  Mwalimu.


Tanzania  imekuwa kimbilio kwa Matibabu  mbalimbai ya magonjwa kwani  wageni kutoka nje ya nchi wanakuja kutibiwa nchini humo zikiwemo nchi ya Malawi,  Zambia, Na Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo hivyo  Fedha za kigeni hupatikana kupitia Wizara ya afya.


Ametoa  pongezi  kwa Watumishi wa afya Mkoa wa kagera  kwa kuweza kushirikiana na serikali katika kuhudumia watu wenye ugonjwa wa  Murbug  ambao ulitokea mwaka jana mkoani Kagera huku baadhi ya magonjwa  mbalimbali yakiwemo Mafua, Malaria,  na ukimwi vimepungua.


Mwaka huu 20224   wizara  ya afya kwa kushirikiana na serikali  kwenda kuboresha huduma za afya  na kupunguza magonjwa  yanayoambukiza na yasiyoambukiza.


Waziri  ummy  ametoa  wito  kwa wananchi  kuacha kutumia vitu vyenye  sukari, nyingi  na chumvi hivyo wananchi ni vyema kuwasikiliza watu wenye Dhamana  ya Afya akiwemo Dkt Janabi ambaye anahamasisha afya.




Post a Comment

0 Comments