MELI YENYE UREFU WA MITA 294 YAWASILI NCHINI IKIWA NA WATALII 2400

 


Na  Sheila  Ahmadi


Mamlaka ya Usimamizi wa bandari  TPA  imepokea meli  kubwa ya  watalii  aina ya   Norwegian Dawn  yenye urefu wa mita 294  huku i kipitia  bandari tofauti tofauti  ikiwemo bandari ya mombasa hadi kufika nchini Tanzania  ambapo uwezo wa meli hiyo ni kubwa inaweza   kubeba abiria 4000 ambapo baadhi ya watalii waliosafiri na meli hiyo ni 2400 kuja nchini  Tanzania.


Hayo  yamesemwa  na Mkurugenzi  wa bandari  ya Dar es salam   Mrisho  mrisho  mara  baada  ya mapokezi ya meli hiyo ambapo  amesema kuwa watalii ambao wamefika kwenye meli hiyo ni zaidi ya  2210 huku baadhi ya wengine wakiwemo wafanyakazi wa meli hiyo ni  1000 hivyo  meli hiyo ina ukubwa wa hali ya juu.


Ukubwa wa meli hiyo  ina urefu  wa kina  294  hivyo  kupitia   Royal  tour    imezaa  matunda na imeweza  kuleta  watalii   mbalimbali   kutoka  nchi  Za  nje kuja   Tanzania kutembelea vivutio vya watalii ikiwemo mbuga ya selou,   Fukwe za bahari, na makumbusho yaliyopo jijini  dar  es salaam.


" Sisi  kama bandari  Tunafurahi  kama ambavyo wao wenyewe wamefurahi  kuja kutembea nchini  Tanzania  kwa huduma ambazo wamezipata bandarini kwa kushirikiana na kapteni ambaye amehusika kupokea meli hiyo na kuweza kuhakikisha  usalama unaimarika kwa watalii hao.


Meli  hiyo  ikitoka bandari  ya dar  es salaam itaelekea  Msumbiji  kwenye  bandari nyingine huku dare salaam ikiweza kukaa  kwa mda mchache huku  ulinzi  na usalama ukiwezeshwa kwenye maeneo  yote ya bandari hiyo   ili watalii hao waweze kufanya  utalii ulio bora zaidi


Kwa  bandari  ya Dar  es  salaam  ni mara ya kwanza kuweza kupokea  meli kubwa na yenye urefu wa  kina  kirefu hivyo  mamlaka ya bandari  inajivunia  kuweka maboresho ambayo yanafanywa katika bandari hiyo na kuweka mlango ambao meli hiyo  imepitishwa hivyo  matarajio yetu ni kuweza  kuhudumia  meli zenye urefu wa mita 305.   "Amesema  mkurugenzi  Mrisho"


Kwa  upande  wake  Mkurugenzi  wa  huduma za meli  kutoka bandari zote nchini  zikiwemo bandari ya Tanga Mtwara,  na Dar es salaam  Ndugu   Mwengamno  amesema meli  hiyo inahudumia mizigo na abiria  ambapo mamlaka ya bandari Tanzania TPA  kwa kushirikiana na menejimeti imeweza kuboresha  bandari kwa kiasi cha kuweza kupokea meli  zenye kina kirefu.


Kwa  kushirikiana na waongozaji wa meli nchini wameweza kuweka mazingira wezeshi ya kupokea bidhaa kutoka kwenye  meli na bidhaa mbalimbali yakiwemo  magari  na rasilimali za watu hivyo bandari ya dar  esa laam,   Tanga na mtwara  yatakua na ushindani wa kibiashara.







Post a Comment

0 Comments