BODI YA WAHANDISI. NCHINI YAADHIMISHA MIAKA 21

 

Na Sheila Ahmadi


Bodi ya Wahandisi  nchini yaadhimisha  miaka 21 ya utendaji kazi ikiwa  na lengo mahususi ya kuweza kuhamasisha wahandisi  wadogo ambao wako vyuoni  na kuwaanda vyema katika mafunzo mbalimbali ya kazi za uhandisi  nchini .


Akizungumza jijini Dar esalaam mara baada ya mafunzo ya wahandisi  wadogo Msajili wa bodi ya usajili  Wahandisi  Tanzania.  Mhandisi  Benard kavishe amewataka. Wahandisi ambao wanatoka vyuoni kabla ya kupata ajira wawe na uwezo wa kufanya kazi wenyewe na kusimamia miradi ambayo wamepewa hususani kwa miaka mitatu.



Mpango huu umekua wa mafanikio toka mwaka 20003. Hivyo kwa sasa tumefanikiwa kutimiza miaka 21 hivyo katika siku hizi tatu za mafunzo tumeweza kuanzisha miradi miwili huku mradi mmoja tumepewa kama msaada.kutoka serikali ya. Norway ambao unaenda kunufaisha miradi yote  miwili kutoka Zanzibar na Bara kwani zanzibar nako kuna miradi lakini kwa sasa tumeshirikiana katika kupokea  Masada.

"Adha  chama cha wanawake. Wahandisi Tanzania wamepewa  majukumu katika msaada ule wa norway kwa ajili ya kuendeleza masomo ya Sayansi. Huku tukiendelea kufanya mafunzo kwa wale ambao ni wanufaika hivyo tumefanya mafunzo ya watu Takribani 500 kwa wale ambao wapo kwenye mradi na ambao hawapo kwenye mradi


Kuna baadhi ya watu wamedandia kwenye mradi huo katika kufanya mafunzo hayo huku tukitoa pongezi kwa wadau wetu wote kwani bila wadau jambo hilo lisingeweza kufanyika hivyo ni lazima kupata sehemu ambazo  zitakua wezeshi kwenye utendaji wake na tumepata nafasi. Ya kuchakata wadau kwa ajili ya kuwashukuru. " Amesema Mhandisi kavishe"


Hata hivyo mbegu ya uhandisi inatakiwa kupandwa mapema kuanzia kidato cha kwanza na pili kwani inapofika kidato cha pili baadhi ya wanafunzi wanajigawa kwenda sanaa na sayansi hivyo tunakiwa kuandaa watoto wakiwa wadogo kwani uhandisi unatakiwa umahiri katika kujifunza hivyo kwa wale walioko sekondari na sana ndoto ya kuwa wahandisi lazima waendelee  kusoma masomo ya sayansi, hesabu na fizikia.




Kwa upande wake mmoja wa wanufaika wa Mradi huo  Mhadhiri kutoka chuo kikuu cha maji  Mhandisi. Nancy. MNduma ameongeza kusema kuwa mimi ni mmoja wa wanufaika wa mradi huo hivyo nawashukuru bodi ya usajili wa  wahandisi nchini kwa kuweza kuadhimisha miaka 21   programu ya  cip ambayo mimi kama mnufaika wa programu hii ya mwaka 2018_ 2021 imekuwa muhimu kwa wahandisi ambao wanatoka vyuoni na kupitia mafunzo maalumu.


Kupitia mafunzo haya tumeweza kupata ujuzi mkubwa ambao unakuwezesha kwenda nje ya nchi kushiriki  miradi mbalimbali ya kujenga Taifa hivyo ujuzi binafsi unaweza kutoka nao kwenye shughuli ambazo unaweza kufanya huko nje pía kukujengea uwezo  wa mitandao ya kutoka mbali

Post a Comment

0 Comments