MKURUGENZI. WA SHIRIKA LA RELI TANZANIA TRC. MASANJA KADOGOSA AELEZA. MAFANIKIO YA RELI KUPITIA MIAKA MITATU YA RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN.

 

Na  Sheila  Ahmadi

Mkurugenzi.  wa shirika la Reli nchini  Tanzania (TRC)  Masanja Kadogosa ameeleza mafanikio ya reli  na  Ujenzi wa Miundo mbinu hiyo  kupitia miaka mitatu ya Rais Dkt Samia suluhu hasani kwa kuweza kutoa fedha  takribani trion 23.3 ambapo tayari shilingi trioni 10 zimeshalipwa kutekeleza Mradi huo wa reli ya kisasa.


Hayo  yamesemwa. Na Mkurugenzi wa shirika la reli Tanzania  Masanja kadogosa  alipozungumza na  waandishi wa Habari na wahariri wa vyombo vya habari nchini jijini Dar es Salaam  ambapo  amesema kuwa zaidi ya Asilimia 70 ya Bajeti ya serikali imewekeza katika Ujenzi wa Reli ya Umeme (SGR) ambapo Endapo Reli hiyo inaenda kupunguza kero ya uondoaji wa Mizigo kwenda kwenye Bandari kwa kutumia Barabara.


" Reli ya SGR ilianza  Awamu ya tatu ya Rais Hayati Benjamin Mkapa,likaanza kutekelezwa na Awamu yatano na kuendelezwa na ya Sita ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan"Amesema  Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania Masanja kadogosa.


Aidha  kadogosa ametoa wito  kwa Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita  waweze kushirikiana vyema ili kuboresha miundombinu wezeshi kwa watumiaji huku  tayari imeanza  kujengwa reli hiyo Kutoka Uvinza mkoani kigoma  hadi Msongati.


Wajerumani walikuwa na wazo la kujenga Reli ya (SGR)  nchini Tanzania hivyo  Rais wa Jamuhuri  ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan ameweza kuziunganisha nchi za Afrika Mashariki katika kuendeleza uchumi wa nchi yetu.


"Tuna  mpango  Madhubuti  kufikia Mwezi  March28 Mwaka huu tunapokea vichwa 5 vya treni vyenye Aina ya Mchongoko  mbele kama tulivotoa taarifa  hapo Awali " Amesema   Kadogosa.


Serikali  yetu imeweza kuingia  mkataba wa Ujenzi wa Reli ya (SGR) Tabora hadi Isaka na Benki ya Dunia .hivyo WanaHabari   ujenzi wa Reli ya SGR kutoka Dar hadi Makotopola tayari Umeshafikia Asilimia 97.


" Kwa Mwaka fedha 2024/25 tunarajia kuanza wa Ujenzi wa SGR katika Mikoa ya Tanga ,Moshi na Arusha.


Naye Mkuu wa Kitengo cha Habari  na Mawasiliano wa Shirika hilo,Jamila Mbarouk  amesema kuwa tumewaita   wanahabari kwenye  Mkutano huu  Dhumuni kubwa ni kuweza kujenga uelewa kwa wanahabari   kuhusu  Mradi huu wa kimkakati ambao unaendelea kutekelezwa na serikali yetu.



Post a Comment

0 Comments