BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO (TADB) WAMETOA MAFUNZO YA MIKOPO KWA WAATALAMU WA KILIMO NCHINI.

 


Na Sheila  Ahmadi

Benki ya  maendeleo. ya kilimo  (TADB) imetoa  mafunzo ya mikopo kwa wataalamu wa kilimo nchini ikiwa na lengo Mahususi la kuweza kuhudumia watu mbalimbali Katika huduma hizo za kilimo   huku washiriki kutoka Burundi wameweza kushiriki Katika mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Benki ya kilimo kwa kushirikiana  na Benki mbalimbali nchini.


Hayo  yamesemwa jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  maendeleo  ya kilimo (TADB) Dkt  Kanaely Nnko amesema kuwa Dhumuni la kutoa mafunzo hayo ni kuweza kwenda kutoa mikopo kwenye sekta nzima ya kilimo kwani tumekuja na wahitimu  Takribani 52.  Kutoka kwenye Benki ya ushirika 20 ambazo zimeshiriki mafunzo haya.


Dkt  Nnko Amesema ni fursa kupata  washiriki kutoka nchi Jirani huku Benki ya 

BOT Academy.  Ambapo wameendesha mafunzo haya na chuo Kikuu cha kilimo SUA Sokoine university of Agriculture, Chuo kikuu cha SAUTI St Augustine University ambao wamekuwa washiriki wetu wazuri tangu Mafunzo yameanza mpaka kufikia siku ya mwisho na kuweza kuhakikisha wahitimu  wetu wa kwanza wamehitimu   na kupata mafunzo "Amesema Dkt Nnko"


"Tumeamua kutoa mafunzo haya  mikoani kote kutokana na wakulima waweze kupata uelewa kuhusu kilimo kimekuwa kikiendesha Mafunzo kama haya hivyo mpaka sasa mfuko wetu wa Garantii umeweza Kudhamini mikopo 270 na mikopo hiyo imetolewa na Benki la shirika hilo. Na walengwa wa kilimo. Wa moja kwa moja .tumeweza kuwafikia takribani  elfu 24.


Kwa upande wake Makamu mkuu wa chuo kutoka chuo cha Benki ya Tanzania mkoani Mwanza  Ephurem   masanguti   Amesema sisi ni sehemu ya Benki kuu tukiwa na majukumu  makubwa ya kuweza kuelimisha   Umma. Ikiwa na pamoja na mabenki. ya Fedha   pamoja na wafanyakazi wa Benki kuu  na Taaluma mbalimbali. Katika kutimiza majukumu yetu Benki kuu ya Tanzania BOT inaelimisha umma na kuchangia dira .


Aidha sisi kama Benki kuu tulipewa majukumu na Benki ya Maendeleo ya kilimo TARB ya kutengeneza  programu kwa ajili ya wakulima wadogo wadogo hususani imeenda kulenga kwenye uelimishaji wa  Mabenki na maafisa mikopo ambao wanasimamia   Benki ya kilimo katika kuweza kutoa mikopo hiyo" Amesema Makamu masanguti".


Naye Afisa mahusiano Mollen Charles kutoka benki ya Absa Amesema kuwa Tumepata mafunzo kwa wiki mbili ya kilimo ambapo tulikuwa na mtazamo kuhudu kuwakopesha  mikopo wakulima wa chini kwani wanachangia katika uzalishaji wa  chakula.

Post a Comment

0 Comments