Na Sheila Ahmadi
Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu HESLB inatarajia kutoa mikopo kwa Wanafunzi 250,000 wa vyuo vya kati na elimu ya juu ili kwenda kunufaika na mikopo katika mwaka wa masomo 2024/2025 ambapo Sh bilioni 787 zimetengwa.
Aidha Idadi ya wanafunzi imeongezeka kutoka 224,056 wa mwaka 2023/2024 ambapo watakaonufaika ni wa shahada za awali, stashahada, stashahada ya umahiri katika mafunzo ya sheria kwa vitendo, shahada za umahiri na uzamivu na ruzuku za Samia.
Hayo yamesemwa jijini. Dar es saalaam na Mkurugenzi. Mtendaji wa HESLB. Dkt Bill Kiwia ambapo amesema kuwa uzinduzi wa msimu mpya wa uombaji mikopo ya Wanafunzi dirisha la kuomba mikopo kwa njia ya mtandao litakuwa wazi kwa siku 90 hadi Agosti 31,2024 na kusisitiza kuwa hawataongeza muda.
"Mkurugenzi Huyo amesema.kuwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Dk. Bill Kiwia, akizungumza wakati wa uzinduzi wa msimu mpya wa uombaji mikopo kwa mwaka 2024/2025.
“Kwa uzoefu wetu siku 90 zinatosha kwa kuwa mwombaji akiwa amejiandaa na nyaraka zote muhimu inamchukua muda wa dakika 40 kukamilisha maombi yake kwa njia ya mtandao. Hivyo, tunasisitiza waombaji wa mikopo kuzingatia muda uliotolewa kwa kuwa hatutarajii kuongeza baada ya Agosti 31,” amesema Dkt Kiwia.
Vilevile. Dkt kiwia Ameongeza kwa kusema mwombaji anatakiwa kuwa na akaunti ya benki na kwamba kwa waombaji wenye namba za nida watapaswa kuziweka wakati wa kuomba mkopo na kama mwombaji hana anaweza kuendelea na maombi bila namba hiyo.
Nitoe wito kwa wanafunzi wanaoomba mkopo kusoma na kuzingatia maelekezo yaliyomo katika miongozo ya utoaji mikopo na ruzuku ambayo tayari imewekwa kwenye tovuti ya bodi hiyo ikiwa katika lugha za Kiswahili na Kiingereza.


0 Comments