HESLB IMEZINDUA RASMI KAMPENI YA "FICHUA"

 

Na  Sheila  Ahmadi

Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB)  imezindua  rasmi kampeni ya fichua  ambayo  inaenda. Kurejesha mikopo  kwa wale ambao walipewa kutoka vyuoni  hivyo bodi ya mikopo tunaenda. Kufichua madeni sugu kwa wahusika ambao walipatiwa mikopo hiyo.


Hayo  yamesemwa  jijini  Dar es salaam  na Mkurugenzi  mtendaji  wa Bodi ya mikopo ya elimu ya juu   (HELSB),Dkt Bill Kiwia, ambapo amesema kuwa  hali ya  urejeshwaji mikopo kwa sasa baadhi ya  wanufaika nchini inaridhisha ambapo sasa wanapokea bilioni 12 kwa mwezi toka bilioni 2.5 mwaka 2016.huku ongezeko la urejeshaji huo  ukiwa umeongezeka kwa kiasi kikubwa.


Aidha. Dkt Kiwia, amesema kuwa  kampeni  ya kuwafichua wanufaika wa mikopo ambao wapo mtaani wasiotaka kurejesha  Mikopo huku wana maisha ya kuweza kurejesha  kwa wakati tumeanzisha kampeni hii rasmi kwa lengo la kuweza kukusanya  mikopo hiyo ili iende kwa vijana ambao wanasoma vyuoni  na kutimiza malengo yao.


"Mwaka 2016 tulikuwa tunakusanya bilion 2.5 kwa mwezi,lakini kwa sasa hali ni nzuri tunakusanya Bilioni 16 kwa mwezi toka kwa wanufaika laki mbili wa mikopo hiyo"Amesema Dkt Kiwia.


Hivyo  Dkt Kiwia,amesema kwa sasa Tanzania inashika nafasi nzuri Barani Afrika kutokana na hali nzuri ya urejeshwaji mikopo hiyo na sisi kama bodi ya mikopo tumeona vyema kuanzisha kampeni hii katika kukamilisha ndoto za vijana nchini na wenye uhitaji.


Dkt  Kiwia,amesema kampeni hiyo ya awamu ya kwanza   itadumu  Takribani kwa miezi miwili itawapa nafasi wananchi kwa watanzania kuwataja wanufaika ambao wapo mitaani ambao hawataki kurejesha mikopo hiyo.


"Kama unamuona mtu unamjua amenufaika. Kupitia mikopo hiyo  unaweza ukataja jina lake,eneo analofanyakazi,chuo alichosoma kwenda kwenye namba 0736665533"Amesema Dkt Kiwia.


Naye. ,Mkurugenzi.  Wa  urejeshaji na urejeshwaji kutoka bodi ya  mikopo CPA George mziray. amesema kuwa  katika kampeni hiyo wanatarajia kuwafikia  Wanufaika zaidi ya elfu hamsini huku wanatarajia kukusanya zaidi ya bilioni mia mbili  nchini.

Post a Comment

0 Comments