Na Sheila Ahmadi
Chuo Cha Bahari Dar es saalam DMI kwa kushirikiana na Chuo cha bahari kutoka Ghana wameandaa kongamano la kitaaluma ambalo litahusisha washiriki mbalimbali kutoka nchini wakiwemo viongozi wa Taasisi, taasisi binafsi, taasisi zisizo za kiserikali, huku watu kutoka Kenya, Comoro, Liberia, Ghana, Nigeria, Italy, na nyinginezo zitashiriki kwenye kongamano hilo.
Hayo yamesemwa jijini Dar es salaam na Mkuu wa chuo cha bahari dar e salaam DMI Dkt Tumaini. Gurumo amesema kuwa kongamano hili la uchumi wa bluu ni la tatu kwani tunaenda kutoa elimu kwa kushirikiana watu mbalimbali katika kuendeleza uchumi wetu kutoka kwenye vyanzo vya maji vikiwemo bahari, maziwa na mito.
"Uchumi wa bluu unajumuisha bahari ya Hindi kwani nchi yetu ya Tanzania tumebarikiwa maziwa makubwa likiwemo ziwa Victoria, Tanganyika na ziwa nyasa hivyo tunaona kwenye uchumi wa bluu tunapata faida mbalimbali za mito na kuweza kutambua matumizi yake ikiwemo kutoa vitoweo kutoka baadhi ya bahari na maziwa nchini kwetu.
Aidha uchumi wa bluu unatupatia usafiri wa majini kwani baadhii ya vyombo vya maji hutumia maji katika kuwezesha uvuvi wa bahari na vingine kutumika katika kusafirisha abiria wanaosafiri kwa njia ya maji na kusafirisha mashehena ya vitu kutoka kwenye maji hivyo maji ni uchumi wa nchi katika maendeleo ya nchi yetu " Amesema Dkt Gurumo".
Nitoe wito kwa watanzania wote nchini katika kushiriki katika kongamano hili tunaloenda kulifanya kwani tutatoa mafunzo na elimu kwa watumiaji wa vyombo vya majini wakiwemo mabaharia kutoka nchini hivyo kila mtu ni mdau wa uchumi wa bluu tunatakiwa kushiriki kwa pamoja ili tuendeleze uchumi wa bluu katika kukuza sekta ya uchumi wetu.
Vilevile Dkt Gurumo ameongeza kuwa. Kongamano hilo litafunguliwa na Naibu waziri mkuu na waziri wa nishati Dkt. Dotto biteko ambapo watalaamu wote kutoka sekta ya bahari, utalii, Bandari, mafuta na gesi , uvuvi watashiriki katika kutoa elimu lengo ikiwa ni kutoa ujuzi kwa watumiaji wa vyanzo vya maji huku kongamano hilo likiwa na kauli mbiu isemayo kuwa " KUIENDEA KESHO KUJUMUISHA UlINZI NA USALAMA WA MAJINI MABADILIKO YA TABIA YA NCHI NA. MAENDELEO YA TEKNOLOJIA KWA UKUAJI WA UCHUMI WA BLUU"


0 Comments