SERIKALI KUPITIA OFISI YA WAZIRI MKUU IMEKABIDHI BOTI YA DORIA (PBSAILFISH ) KWA SHIRIKA LA UWAKALA WA MELI TANZANIA (TASAC) .

 

Na Sheila  Ahmadi 

Serikali  kupitia Ofisi ya Waziri mkuu imekabidhi  Boti ya Doria (PBSAILFISH) kwa  Shirika la Uwakala wa Meli  Tanzania  (TASAC )  ili  kwenda kuweza kukabiliana na vitendo vya kihalifu ikiwemo UVuvi haramu,  na madawa ya kulevya  katika Bahari na Maziwa Makuu ambao unatekelezwa kikamilifu.


Akizungumza Jijini  Dar es salaam  Mara baada ya kupokea Boti hiyo ya Doria Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri  Mkuu   DKt  Jim Yonazi  Amesema kuwa lengo La kukabidhi boti hii  ni kuweza kukabiliana   na  vitendo haramu kwenye Maziwa makuu  na bahari nchini  zikiwemo Uvuvi,madawa ya kulevya, ambapo Doria hizo ni Mwendelezo  wa juhudi za kiserikali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na biashara za magendo.


"Tunatambua kuwa Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mna usimamizi,na uendeshaji nzuri hivyo tumeamua kuja kuwakabidhi ikiwa na pamoja kuweza kuifanyia Matengenezo kinga kwa Wakati hivyo ufanisi utaongezeka katika kazi zenu hususani katika ukaguzi wa meli. Ambazo zinaingia kwenye maji yeti ya ndani. 


Aidha  Dkt  Yonazi  Ametoa  wito kwa TASAC waendelee kufanya kazi kwa karibu na idara ya Menejimenti ya maafa iliyopo ofisi ya Waziri Mkuu. Kwa ajili ya kuweza kuratibu progiramu za uokozi wa majanga ya majanga na usalama. na Bahari kwa Ujumla." Alisema Dkt Yonazi.


Naye  Naibu  katibu Mkuu wizara ya uchukuzi  Bw.  Ludovicky  Nduhiye Amesema kuwa Boti hii kwa shirika letu  La Uwakala wa Meli Tanzania TASAC imekuwa chachu  katika kutimiza kwa vitendo Dira yetu Ambayo imelenga kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye huduma za uchukuzi na hali ya hewa zenye uhakika, usalama na nafuu.


Kupitia  ofisi ya Waziri  Mkuu  kununua boti hii ya kisasa  ni kuweza kuhakikisha TASAC inaweza kushirikiana na wadau wengine katika kutekeleza majukumu ya msingi ya shirika yanayohusu usimamizi wa masuala ya ulinzi, usalama udhibiti wa uchafuzi wa mazingira ya Bahari ambao unatokana na uchafuzi wa Meli.


Vilevile   Bw  Nduhiye  ameongeza kuwa Boti hii itasaidia kwenda. Kuimarisha ulinzi katika Bahari kuu kwani ni ya kisasa na yenye kasi na ina  ukubwa ambao itawezesha kufanya ufatiliaji wa har aka na Doria katika maeneo yetu.   

Kwa upande  wake   Mkurugenzi  Mkuu wa Shirika La  Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw  mohamed  Salum  amesema kuwa serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ilk kuweza kuimarisha usalama wa usafiri majini hivyo boti hii inayokwenda kuikabidhi TASAC hivyo  boti hii  inaenda katika maeneo ya Bahari na Maziwa makuu ikiwa ni kuhitaji mikakati  thabiti ya udhibiti wa shughuli hizo.


Aidha serikali  imeandaa Mwongozo wa Taifa wa kuweza kukabiliana na vitendo vya kihalifu katika Bahari na Maziwa makuu wa mwaka 2022 ambaoni mahususi kwa ajili ya kuzuia na kukabiliana na shughuli haramu za baharini.


Pia Bodi ya Menejimenti  ya Shirika La Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) tunaishukuru serikali ya awamu ya sita kwa  kuwa Mstari wa mbele katika kuhakikisha wananchi wanaendesha shughuli Za  majini huku wakiwa katika hali ya usalama.



Post a Comment

0 Comments