#KAZIINAONGEA
Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imekuwa na mchango mkubwa katika kurejesha uhuru wa Habari nchini.
Kwa mujibu wa ripoti ya Reporters Without Borders (RSF) hadi kufikia mwaka 2023 Tanzania ilikuwa katika nafasi ya 143 ya viwango vya Uhuru wa Habari duniani.
Hata hivyo juhudi za kisera na sheria zilizochukuliwa na serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kama vile kurekebisha baadhi ya sheria za vyombo vya habari na kuruhusu vyombo vilivyofungiwa kurejea hewani, zimeisaidia Tanzania kupanda hadi nafasi ya 97 kwa mwaka huu.
Hatua hii inaifanya Tanzania sasa kuwa ya kwanza kwa Uhuru wa vyombo vya Habari kwa ukanda wa Afrika Mashariki.
Aidha upatikanaji wa Habari na uhuru wa kutoa maoni kwa Watanzania umekuwa ni wa kiwango cha kuridhisha.
Hali hiyo imeondoa malalamiko ya kuminywa kwa haki hiyo ya kupata taarifa.
Rais Samia hajaishia katika kuinua uhuru wa Habari nchini, pia amepambana kuinua uchumi wa vyombo vya Habari na wanahabari.
Mara kadhaa Rais Samia amekuwa akizitaka Taasisi na Idara mbali mbali za serikali yake, kulipa madeni yote wanayodaiwa na vyombo vya habari nchini kulingana na mikataba ya kazi waliyoingia kabla ya Desemba 24, mwaka huu.
Hivi karibuni Rais Samia amerejea agizo hilo wakati akifungua Kongamano la pili la Maendeleo ya Sekta ya Habari nchini, lililokuwa likijadili masuala mbali mbali na kutoa maelekezo ya madeni ya vyombo vya Habari kulipwa.
Rais pia ameyagusa maslahi ya mwandishi mmoja mmoja, ambapo alivifungulia baadhi ya vyombo vya Habari vilivyofungiwa yakiwemo magazeti, ambayo kufungiwa kwake kulisababisha baadhi ya waandishi kupoteza ajira.
Ikumbukwe kuwa, kwa kipindi kirefu, Waandishi wa Habari wamekuwa wakifanyakazi katika mazingira magumu ikiwemo kutolipwa stahiki zao pamoja na kukosa uhuru katika kufanya kazi zao.
Dhamira ya Rais Samia, imekuwa chachu hata kwa viongozi wengine kuhakikisha wanasimamia kile alichokiasisi.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa yeye ni miongoni mwao na amesema Serikali imeandaa mkakati wa Mawasiliano ya Taifa ili kuhakikisha wadau katika ngazi zote wanapata taarifa za

0 Comments