MAKAMBA AWAVAA WANAOKAFIFU MWENGE WA UHURU




Waziri wa Nishati January Makamba amesema kuwa  kumekuwa  na  hoja na mjadala kwabaadhi ya wanasiasa hasa wa upande wapili wakidai mwenge wa uhuru umepitwa na wakati. 



Makamba amesema kuwa Mwenge ni Tunu ni nembo ya Taifa hivyo na kwa

kusema mwenge unasumbua watu   ni sawa na kuitusi nchi  ya Tanzania.



Makamba ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bumbuli ameyasema hayo mara baada

ya mwenge kufika katika Jimbo hilo, ambapo mwenge huo umezindua  na

kukagua miradi 9 yenye thamani ya sh.779.1 million



 " Tukiwa na mawazo na mtazamo huo tunaitusi historia ya nchi yetu

kwani nchi yetu ilipopata uhuru, hotuba ya kwanza ya Baba wa Taifa

Mwalimu Nyerere amesema sasa tunawasha mwenge iliuangaze nchinzima, "

amesema  January Makamba



Alisisitiza kuwa mwenge wa uhuru ni kielelezo cha uhuru, utaifa wetu,

ni ndoto zetu, na ni kiunganishi cha watanzania pamoja na kuwa

utamaduni  na kielelezo cha utaifa wa Tanzania.



Alifafanua kuwa kila nchi ina urithi wake na utamaduni zake na kila ukoo

una tamaduni zake na kwamba kwa Tanzania moja ya urithi wake ni Mwenge

na  ndiyo maana upo kwenye nembo ya taifa na hata kwenye  sarafu.

Post a Comment

0 Comments