Na: Sheila Ahmadi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassani atafungua mkutano wa kwanza wa kitaifa wa dira ya maendeleo ya taifa utakaofanyika jijini Dar es Salaam Disemba 9 lengo la mkutano huo ni kupokea na kujadili taarifa za tathmini ya utekelezaji wa dira hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Waziri wa Nchi, OFisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo amesema taarifa hiyo ya kitafiti inaenda kutekeleza dira ya taifa ya maendeleo mwaka 2025, huku mambo mengine yakitekelezwa na kuonesha kuwa pato la Mtanzania limeongezeka kutoka dola za kimarekani 1,200 kwa mwaka 2022.
Aidha waziri Kitila amesema Tanzania imefikia asilimia 124 ya kujitolea kwa chakula huku ikilinganishwa na lengo la kufikia asilimia 140 ifikapo mwaka 2025 hatua hiyo imewezesha Tanzania kukabiliana na njaa kwa mikoa na wilaya zote nchini .
"Mtandao wa barabara za lami na zege (Paved Roads ) katika mikoa umeongezeka kutoka Kilomita 4 , 179 mwaka 2000 hadi kufikia kilomita 11, 966.8 kwa mwaka 2023 na mafanikio mengine ni pamoja na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 760 kwa vizazi hai 100, 000 mwaka 2000 hadi kufikia vifo 104 na mwaka 2022 ikiwa tumevuka lengo la kufikia vifo 265 ifikapo mwaka 2025.
Kutokana na mkutano huo Rai samia atazindua rasmi timu kuu ya kitaalamu ya dira (National vission core Technical Team na kamati ya usimamizi wa dira (Natonal vission steering comitee) pamoja na nyenzo Za kidigitali ambazo zitaenda kutumika katika kkusanya maoni ya wadau.
Hata hivyo amesema kutokana na zoezi la kuandaa dira mpya ya maendeleo iwe jumuishi na shirikishi ambapo mkutano huo utahudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka pande zote za nchi wadau hao wakiwemo viongozi wakuu wa serikali ya tanzania serikali kutoka Zanzibar, Mawaziri, makatibu wakuu, na wakuu wa mikoa na Taasisi nyingine binafsi.
Ametoa wito kwa wananchi kuweza kufatilia mchakato wa kuandaa dira hiyo mpya na kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni yao kuhusu Tanzania waitakayo katika miaka ijayo.



0 Comments