ZPRA NA PURA WAWEKA MIPANGO MIKAKATI KATIKA KUKUZA SEKTA MAFUTA NA GESI.






Na   Sheila   Ahmadi


Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli na Gesi Asilia (PURA) pamoja na Mamlaka ya udhibiti wa utafutaji na uchimbaji wa Mafuta na Gesi asilia Zanzibar (ZPRA)   zimekutana na kuweka mipango  mikakati mbalimbali  Jijini  Dar  es  saalam  na kuweza   kuendeleza sekta ya Mafuta na Gesi asilia Nchini na kuendeleza uchumi wa nchi


Hayo  yamesemwa  Jijini  Dar  es salaam katika mkutano  huo alipokua  akizungumza  na wanahabari    Mkurugenzi   mkuu  wa pura  mhandisi Charles  Sangweni    ambapo  amesema kuwa  mkutano huo una  Dhamira  ya kuwa na mipango mahususi   ya kukuza na kuendeleza sekta  ya Mafuta na Gesi asilia kwa pande zote mbili za Muungano, na kuwekeana mikakati thabiti ya kutangaza na kutafta wawekezaji wa vitalu vya mafuta na gesi.


"Katika mkutano huu  tumekutana ili tuweze  kupanga  mikakati  katika kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu ili tuweze kudhibiti na kuendeleza sekta hii muhimu kwa ajili ya Maendeleo ya Taifa letu,tunatumaini baada ya kikao hiki tutaainisha mikakati yetu na kuifanyia kazi ipasavyo" Amesema Mhandisi Sangweni.


Naye    Mwenyekiti wa Bodi ya PURA Khalfan Khalfan ameongeza  kuwa  ushirikiano wa PURA na ZPRA utaenda  kusaidia katika  kujenga mahusiano ya muda mrefu na kwenda  kuhakikisha kuwa  wawekezaji wanapatikana Tanzania huku  wakiendelea  na ushirikiano katika kutoa huduma kwa wananchi  wote.





Mwenyekiti   Khalfan   Amesema  kuwa  ushirikiano huo unaenda  kuleta  manufaa endelevu  kwenye bodi zote mbili( PURA na ZPRA ) na kuwezesha   kutaweza kutangaza vitalu vinginevyo  na kuweza   kupata wawekezaji wengi hivyo sekta ya Mafuta na Gesi asili itazidi kukua nakuleta maendeleo kwa Taifa."  Amesema   mwenyekiti   Khalfan


kwa  upande  wake  Mwenyekiti wa bodi  kutoka taasisi ya Utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia Zanzibar Ali Mirza amesema kwamba kikao hicho kimefanyika kwa mara ya kwanza ili kuweza  kujadiliana kwa pamoja nakuweka mikakati ya pamoja ya kunufaika na rasilimali ya Mafuta na Gesi asilia.


Ameongeza kuwa ushirikiano  huo unaenda kuleta tija kwenye bodi zote  mbili  PURA  na ZPRA na kuweza kutangaza  vitalu vyote katika kuvutia wawekezaji  wengi nchini  hivyo sekta hiyo  ya mafuta na gesi  asili  inaenda kuleta manufaa kwa Taifa.

Post a Comment

0 Comments