RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSANI KUFANYA ZIARA NCHINI KOREA.

 

Na Sheila Ahmadi

Rais  wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt samia suluhu hassani anaenda kufanya  Ziara ya kikazi. Nchini korea huku ziara hiyo ikiwa na dhamira ya kuendeleza  ushirikiano  baina ya Serikali ya Tanzania na Korea ikiwemo Elimu, Afya, na miundombinu  hivyo ziara hiyo inaenda kuleta Mafanikio mbalimbali nchini kwetu. Tanzania


Hayo Yamesemwa  Jijini  Dar es salaam  na Waziri. Wa mambo ya nje na ushirikiano  wa Afrika mashariki  January Makamba mara baada ya kuzungumza na wanahabari ambapo amesema kuwa  tarehe 30 mwezi huu Rais Dkt samia atafanya ziara nchini korea hadi tarehe sita kwa mwaliko rasmi kutoka kwa rais wa nchi hiyo kwani sisi na watu wa korea tuna ushirikiano mkubwa kwa miaka 32.Kupitia  Elimu,  Afya, na Miundombinu.


Kwenye ziara hiyo Dkt samia atafanya mazungumzo na kusaini mikataba mbalimbali ya  ushirikiano  kati ya Tanzania na Korea mikataba hiyo ikiwemo Hati ya makubaliano kati ya Taasisi ya Madini Tanzania. GST na Taasisi ya miamba nchini korea. Hivyo ushirikiano huo unahusu utafiti, uchoraji ramani, rasilimali na uchoraji  wa maabara .


"Mkataba wa pili ambao unaenda kusainiwa kati ya Rais Samia na rais wa korea ni ushirikiano wa uchumi. Wa bluu, huku mkataba wa tatu ukihusu kwenda kutambua vyeti vya Mabaharia  na tutaweza kusaini  Tamko la pamoja kuhusu siasa  na makubaliano ya hati ya Madini, Viwanda na biashara  " Amesema Waziri makamba 


Aidha  Waziri  Makamba ameongeza kuwa kuhusu madini kwenye mkakati tutasaini  mkataba katika kuwezesha  kuchambua, na Kufanya Mkakati na shirika la madini   Tanzania  STAMICO ,  na shirika la ukarabati  wa madini nchini korea 


Hata hivyo Mkataba mwingine ni Msaada wa fedha kutoka benki ya Exim nchini korea  na serikali ya  Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambao unaenda kupelekea nchi yetu  kupata msaada    na mikopo nafuu Takribani dola mbili nanusu vilevile  tunaenda kushirikiana na chuo kikuu kutoka nchini korea katika kuendeleza. Huduma za usafiri wa anga nchini

Post a Comment

0 Comments