DC MPOGOLO AMEPONGEZA TAASISI ZA OSHA, ZIMAMOTO, DAMU SALAMA KATIKA KUADHIMISHA KUMBUKIZI YA MAAFA NCHINI.

 

Na  Sheila  Ahmadi

Mkuu  wa Wilaya  ya ilala Mhe. Edward  mpogolo ametoa pongezi kwa mashirika ambayo yameweza  kuadhimisha maadhimisho  kwenye usawa na haki za kibinadamu nchini.


Hayo  yamesemwa Jijini. Dar es salaam  na Mkuu wa wilaya ya ilala Edward  Mpogolo mara baada ya  maadhimisho ya  kumbukizi ya maafa yaliyowapata baadhi ya Wananchi nchini  ambapo   amesema kuwa mashirika yote ambayo yamejitokeza kwenye maafa na uokoaji ni jambo muhimu kwa Taifa kwani tunatakiwa kujenga Taifa na kukuza uchumi wa nchi.


Aidha Mpogolo ameongeza kuwa katika maadhimisho haya yanalenga zaidi kumbukizi na kuwapa  wale wote wanaojitoa katika harakati za kuwapigania binadamu wengine kwa hali na Mali ikiwemo OSHA, save the children, Red cross, Zima moto na damu salama.


Naye   afisa uhusiano kutoka Wakala  wa salama na Afya mahala pa kazi OSHA Eleuter Mbilinyi amesema kuwa sisi  kama Wakala wa usalama na Afya  mahala pa kazi tunashirikiana  na wadau wengine katika utoaji wa Elimu  ya maafa na kuhakikisha  kuwa mazingira ya kazi yanakuwa salama .


Vilevile OSHA tunashiriki  katika kuwatengenezea wafanyakazi mazingira Bora na salama na kutambua umuhimu  wao katika kujenga uchumi wa nchi , na  kufanya kazi kwenye  mazingira mazuri,hivyo  vifaa na utekelezaji wa ufanyaji wao kuhakikisha una kuwa wenye weredi mkubwa.

Post a Comment

0 Comments