RC MKOANI LINDI AMEUTAKA UONGOZI WA CHUO CHA BAHARI DAR E SALAM (DMI) KUENDELEA KUJENGA TAWI LA CHUO.






Na Mwandishi  wetu

Mkuu wa Mkoa wa Lindi  Bi. Zainab Telack ameutaka uongozi wa chuo cha bahari Dar es Salaam (DMI) kuhakikisha wanaendeleza eneo walilopewa na mkoa huo kwa kujenga tawi la chuo hicho.


Bi  Taleck amesema hayo  ofisini kwake mara baada ya  kuzungumza  na uongozi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam(DMI)  huku ameutaka  uongozi wa chuo hicho  kueleza  mpango wa kutoa mafunzo ya usalama kwa wavuvi mkoani humo.


“Mkoa wa Lindi unawavuvi wengi na asili ya watu wa Lindi  ni Uvuvi na Kilimo hivyo ni muhimu kwa chuo chenu kujenga tawi hapa, eneo tumewapa na tupo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kuhakikisha wavuvi wanapata elimu stahiki ili kukuza uchumi wa Mkoa wa Lindi na taifa letu” Alisema Taleck


Kwa Upande wake Mkuu wa chuo cha DMI Dkt.Tumaini Gurumo   amesema kuwa lengo la kufika ofisini kwa mkuu wa mkoa huo ni kueleza  mpango wa chuo hicho kuanza kujenga kituo cha mafunzo ya usalama katika utafutaji na uchimbaji wa gesi pamoja na kuendelea kutoa elimu ya uvuvi salama .


“Tunaushukuru sana Uongozi wa Mkoa ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa kwa kutupokea mimi na wenzangu pia kwa kutupatia eneo la kujenga tawi la chuo chetu, hivyo tunaendela kukamilisha taratibu mbalimbali za kuanza ujenzi huo” Alisema Dkt. Tumaini.


Aidha viongozi  kutoka chuo cha bahari DMI wameweza kuhudhuria  wakiwemo   Mkuu wa chuo  kutoka DMI Dkt. Tumaini Gurumo   hivyo DMI tutakuwa mkoani Lindi kwa siku nne tukiendelea  kutoa elimu kwa wavuvi na  kutembelea shule mbalimbali za mkoa huo.ili kuweza  kutoa elimu ya fursa za masomo yanayohusu bahari kwa wanafunzi wa shule za Sekondari ili wajiunge na chuo hicho ambacho makao makuu yake yapo jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments