WIKI YA AZAKI KUFANYIKA JIJINI ARUSHA SEPTEMBA 9.

 

Na  Mwandishi wetu

Kuelekea Wiki ya Azaki (CSO )  Kufanyika September 09 hadi 13 Mwaka huu  Jijini Arusha Huku Baadhi ya taasisi zitashiriki zikiwemo ubongo kids, FCS   pia  matukio mbalimbali  yatafanyika  kwenye kutoa ujumbe na  elimu kwa umma.


Hayo yamesemwa jijini Dar e es salaam na  Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi   Christoffel - Blindenmission kutoka  (CBM) Nesia Mahenge ambapo  Amesema kuwa  Wiki ya Azaki mwaka huu inaenda kufanyika  kwa mara ya sita mfululizo na imekuwa na mwitiko mkubwa kutoka kwa wadau na wanachi kwa ujumla.


" Kupitia wiki hiyo tunategemea  kutoa elimu kwa wananchi hususani kwa makundi ya vijana,wanawake na wenye ulemavu.


Naye  Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society (FSC) Justice Rutenge amesema kauli mbiu ya mwaka huu ni voice,vision & value ikilenga kutoa kipaumbele na thamani kwa mawazo ya maoni ya wananchi juu ya Mstakabali wa maslai ya Taifa ikiwemo Dira ya maendeleo ya Taifa.


Aidha Rutenge  amesema kuwa Katika wiki ya Azaki wanasisitiza kila mtu ashiriki katika kutengeneza dira ya taifa na kutengeneza thamani ya malengo ya taifa kwa pamoja.


Hivyo  Licha ya utofauti wa mawazo ulipo katika jamii ni lazima tufikie malengo ya kuhakikisha tunapata mawazo ya pamoja na kuwa na Dira ya pamoja.


Vilevile  ametoa wito kwa  watanzania kuweza  kushiriki katika wiki ya Azaki ili kujifunza mengi na kushirikiana kwa pamoja katika kuchagiza maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.


Kwa upande wake  Mtendaji kutoka  Ubongo kids Mwasi umwe amesema kupitia Taasisi yao wamewafikia Watoto milion 42, hivyo wamekuja kushirikiana na CSO ili kuwafikia wengi zaidi na ni mara yao ya kwanza na wanaamini ni fursa ya kuwafikia watu wengi na kujenga maslai bora ya Taifa kwa pamoja

Post a Comment

0 Comments