SHIRIKA LA RELI TANZANIA (TRC) IMEZINDUA KAMPENI YA KUANZA KUTOA HUDUMA YA USAFIRI WA TRENI ZA SGR RASMI DAR _MOROGORO JUNI 14.

 

Na  Sheila  Ahmadi

Shirika la Reli Tanzania  TRC imezindua  rasmi kampeni ya kuanza kutoa huduma ya usafiri wa  treni za kisasa (SGR)   kutoka Dar es salaam hadi mkoani morogoro mwezi juni tarehe 14 ambapo shirika hilo limesema kuwa ujio wa treni hizo za kisasa hazitoweza kuzuia  vyombo vingine vya usafiri ikiwemo Mabasi yaendayo mikoani na Treni ambazo zilikuwa zinatumika kipindi cha nyuma kwani treni hizo zinasaidia katika kusafirisha  abiria kutoka Dar es salaam kwenda mikoa jirani ikiwemo  morogoro, na kigoma.


Akizungumza. Jijini Dar es salaam  Mkurugenzi. Mtendaji  wa shirika la Reli Tanzania  (TRC)   Masanja  Kadogosa amesema kuwa  leo tunazindua rasmi kampeni hii ya kuanza kutoa huduma za treni ya kisasa kutoka Jijini Dar es salaam kwenda. Mkoani morogoro  juni 14 safari zetu zinaenda kuanza rasmi hivyo  watanzania  tunatakiwa kupanda treni zetu  kwa bei ya shilingi elfu 13000 hivyo  tunawakaribisha katika kupanda treni zetu na kupatiwa huduma bora pindi tuwapo  kwenye  usafiri huo wa Treni.


Kampeni hii ya uzinduzi Ina lengo ya kutoa huduma  za SGR ikiwemo na ulinzi kwenye treni  hizo pia  sisi kama shirika tunaomba  wananchi tushirikiane katika kutunza. Miundombinu kwani treni hio ni Mali ya watanzania na imejengwa kupitia kodi za. Watanzania  kwa kutumia huduma za TRC  ili liwe pato la kitaifa pia tutaangalia ubora wa miundombinu na usalama wa abiria  "Amesema Mkurugenzi kadogosa .


"Sisi  kama Shirika tumejipanga kuanza safari. Za Dar es salaam kwenda Dodoma mwezi  julai  25 Mwaka huu. 2024  huku tukiendelea  kuchukua hatua kadhaa ikiwemo hii ya Tarehe 14 juni  katika kuanza  kutoa safari kupitia treni hiyo hivyo katika kutimiza Agizo La Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt samia suluhu hasani  shirika linatoa pongezi kwa kuweza kutoa huduma  ya Treni katika viwango vya kimataifa SGR. Kutoka Dar es salaam kwenda morogoro  tarehe 14 juni  mwaka huu. Huku uzinduzi huo ukiwa na Kaulimbiu isemayo kuwa  TWENDE TUKAPANDE  TRENI  YETU , TUITUNZE, TUITHAMINI.


Aidha  kuanza  kwa safari hizi  kutoka Mkoani Dar es salaam kwenda mkoani morogoro. Ni sehemu ya kuendelea kujifunza  kupitia Teknolojia mpya nchini na kujiridhisha na mifumo mbalimbali kabula ya kuanza safari rasmi za kutoka Dar es saalam kwenda Dodoma ifikapo tarehe 25 mwezi julai na kuanza safari baada ya shirika kujiridhisha na Miundombinu, vitendea kazi  kwa maana ya vichwa vya mabehewa .


Vilevile Kadogosa  Ametoa pongezi  kwa Rais Dkt Samia suluhu na serikali kwa ujumla kwa kutumia  utashi wake wa kisiasa kwani alitoa a had I kwa watanzania kuwa atamalizia vipande vya ujenzi ambavyo Amelita na kuanzisha vipande vingine hivyo serikali yetu imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo ya kisasa ikiwemo ujenzi wa makotupora .


Kwa upande wake Mkurugenzi  kutoka benk ya Tanzania commercial benk (TCB)  Adam  mihayo.  amesema kuwa tuna furaha kubwa katika kushirikiana na shirika hili kwani ni muda mrefu sasa tunashirikiana katika mambo mbalimbali katika.kukuza uchumi wa nchi yetu kutoka kwenye shirika hili hivyo mimi kama Mkurugenzi wa benki ya TCB tumeaminiwa katika utendaji kazi kupitia kwenye utendaji wetu.


"Tumeingia kwenye makubaliano katika kuweza kutoa huduma kwa watumiaji wa Reli hiyo  pia tukio hili limekuwa la kihstoria kwenye nchi yetu katika.kutimiza maono ya muda mrefu ya Rais Dkt samia kwa kutuletea Treni za SGR  kwani reli yetu ni ya kwanza Afrika Mashariki ." Amesema Mkurugenzi mihayo.


Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Tehama kutoka TRC Lilian Msele ameongeza kuwa tuna end a kutoa huduma za tiketi kwa kontrol namba kwa abiria  lengo ikiwa ni kuepukana na changamoto ndogondogo pia abiria ambao wanaenda kutumia treni hizo wasiwe na mizigo mikubwa zaidi ya kilo 30 na hatutoruhusu  kubeba vyakula lakini watoto chini ya miaka 5 tunaruhusu kubeba maziwa na uji

Post a Comment

0 Comments