HEINEKEN BEVERAGE IMEINGIA MAKUBALIANO NA KAMPUNI. YA MABIBO KUPITIA KWENYE USAMBAZAJI WA BIA.

 

Na  Mwandishi  wetu

Kampuni  ya Heineken Beverage imeingia makubaliano na kampuni ya kitanzania Mabibo bia kwa ajili ya usambazaji wa bia ya Windhoek inayozatengenezwa  nchini Namibia.



Hayo  yamesemwa  jijini  Dar esalaam na  Meneja kutoka  Kampuni ya Heineken Obabiyi Fagade mara baada  ya kuzungumza. Na wanahabari  ambapo  amesema kuwa  lengo la kuingia ushirikiano huo ni mkakati mahususi wa kusaidia biashara za ndani na ukuaji wa uchumi  nchini Tanzania na kupata fursa za ukuaji katika ya kusini mwa Afrika.


"Ushirikiano huo na Mabibo bia ,wines na spirits ni kufungua ukurasa  mpya kwa kuunganisha utaaalamu wetu wa Kimataifa Kama Heineken na ujuzi mkubwa walionao katika soko la ndani,tuna uhakika katika uwezo wetu wa kuwasilisha bidhaaa na huduma za kipekeee kwa watej wetu Tanzania";,amesema .


Aidha  Heineken imedhamiria kutoa  huduma za kipekeee kupitia vinywaji vyenje ubora wa hali ya juu ambavyo vinakizi ladha ya watumiaji.


Kwa. Upande  wake  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Bia Jerome Rugilamalila  amesema  mkataba huo wa kibiashara umekuja baada ya kampuni ya Mabibo na Namibia Breweries kukubalina kuvunja mkataba walioingia mwak 2008.



Post a Comment

0 Comments