ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA KUSAMBAZA TAARIFA ZISIZO ZA KWELI MTANDAONI

 


Na  Mwandishi  wetu 

Jeshi  la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata  Amos Lutakulemberwa Lwizamiaka mwenye. Umri wa miaka  54 mkazi wa Tegeta Wazo Kinondoni kwa tuhuma za kusambaza taarifa zisizo  za kweli  kwenye mitandao ya kijamii kuwa binti anayedaiwa taarifa zake kutoka mitandaoni hivi karibuni mwezi Agost 2024 kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji kwa kubakwa na kulawitiwa amekutwa amefariki suala ambalo sio kweli


Akizungumza  jijini  Dar  es salaam   Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam SACP Muliro Jumanne Murilo  Amesema kuwa kupitia  jeshi  la polisi  limeweza  kumkamata  Amos Lutakulemberwa  ambae ametoa  taarifa ya kufariki kwa binti ambaye amefanyiwa ukatili wa kinjisia ambapo sio jambo la kweli


" sisi  kama  jeshi  tunatoa  wito kwa wananchi katika  kujiepusha na kutoa  taarifa za uongo zenye malengo ya kuzusha taharuki katika jamii kwani kufanya hivyo ni makosa lakini litaendelea kuzingatia maoni ya watu ambayo hayakinzani na sheria za nchi," amesema SACP Muliro.


Aidha  SACP  murilo  amesema. Kuwa  hali ya usalama kuelekea mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Yanga na Simba katika Uwanja wa Benjamini Mkapa SACP Muliro ameeleza kuwa Jeshi hilo limechukua tahadhari zote za kiusalama kabla, wakati na baada ya mchezo huo. 


"Usalama utaimarishwa kwa kiwango cha juu. Jeshi linawakumbusha nimarufuku kwa mtu yeyote kwenda na silaha uwanjani isipokuwa vyombo vya dola vyenye jukumu la usalama eneo hilo. Watu watakaojihusisha na vitendo vyakihalifu ndani au nje ya uwanjawatashughulikiwa haraka kwa mujibu wa sheria," amesisitiza SACP Muliro.

Post a Comment

0 Comments