Na Sheila Ahmadi
Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB). Imebadilishana hati
Za makubaliano na Taasisi Kadhaa za kimkakati ambazo zinaenda kutekeleza kwenye utoaji wa taarifa katika kuwasaka wadaiwa sugu wa mikopo ambao walipewa kipindi wako vyuoni na kushindwa kurejesha kwa wakati.
"Bodi ya mikopo inatoa rai kwa wanufaika wa mikopo Hiyo ambayo walipewa ili waweze kurejesha mikopo kwa wakati ili wengine waweze kwenda vyuoni kuendelea na masomo huku Taasisi Ya Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa NIDA, wakala wa usajili ,ufilisi na udhamini RITA,taasisi za uchakataji wa taarifa za waombaji mikopo kwenye taasisi za fedha CREDITINFO zikiwa tayari kwa majukumu ya kuwasaka wadaiwa hao.
Aidha MKurugenzi Kiwia ameongeza kuwa katika ukusanyaji wa mikopo hiyo tunawakaribisha wadau hawa katika kwenda kufikisha ujumbe huu kwa kutumia Mifumo ya tehama.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi mkuu kutoka
Mamlaka ya vitambulisho vya taifa nida Deusdedit buberwa amesema kuwa tutashirikiana vyema katika kutekeleza makubaliano ya serikali huku taasisi za kiserikali zikiweza kuunganisha mifumo ya tehama katika kutoa huduma kwa wananchi.
Naye Mtendaji mkuu kutoka RITA. Frank kanyusi amesema kuwa tuna jukumu la kutoa vyeti vya uzazi na Vifo katika kuweza kukamilisha suala hilo la wadaiwa hivyo sisi kama Rita tumeweza kujiunga na mfumo wa kieletronik ili kumwezesha kupata Cheti ambapo bodi ya mikopo watahitaji kuona vyeti vya muombaji wa mkopo ili kuhakikisha kuwa ana visibitisho vyote .
Vilevile mtendaji mkuu kutoka CREDITINFO Edwin Urasa ameongeza kuwa wanufaika wa mikopo hiyo ya elimu ya juu waanze kujitokeza na kurejesha mikopo kwa wakati sahihi ili taasisi za fedha ziweze kukopesha wanavyuo wengine ambao wanatarajia kwenda vyuoni hivi karibuni.






0 Comments